• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BARABARA ZA MJINI KATI SENGEREMA KUCHOCHEA MAENDELEO YA WANANCHI

Posted on: August 30th, 2025

Leo Agosti 30, 2025 Mwenge wa Uhuru umekagua na kuweka jiwe la Msingi kwenye mradi wa ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami (Double Surface Dressing) zenye urefu wa kilometa 0.72 unaotekelezwa na mkandarasi MS Jassle Company Ltd kwa Tshs. 474,950,400.

Akiongea na wananchi kwenye mradi huo, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025 Bw. Ismail Ali Ussi amemtaka Mkandarasi huyo kukamilisha ujenzi wa miundombinu hiyo kwa mujibu wa mkataba na kwa ubora unaokubalika ili barabara hizo zirahisishe mawasiliano na kusaidia kuchochea maendeleo.

Bwana Ussi ameipongeza serikali kupitia mfuko wa maendeleo ya jimbo kwa kutoa fedha nyingi chini ya usimamizi wa Wakala wa barabara vijijini na mijini (TARURA) katika kuhakikisha wananchi wa barabara za CCM-Bwawani (0.25) na Pambalu (0.47) ikiwa ni katika kuwaboreshea mawasiliano ili kuboresha huduma za kijamii.

“Serikali inatekeleza mradi huu (Barabara) na mingine mingi kwa sababu nyie wananchi mmekua tayari kupokea, hivyo nawaomba muendelee kuipenda na kuiamini serikali yenu ya awamu ya sita ambayo ipo kwa masilahi ya wananchi wakati wote na itaendelea kuwaletea miradi mingi ya kijamii.” Amesema kiongozi huyo.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga amebainisha kuwa serikali imejenga barabara hizo za mjini kati ili kuupa hadhi mji wa Sengerema na kwamba zitakapokamilika zitawasaidia wananchi kuwafikisha kwa urahisi na haraka katika maeneo ya huduma za kijamii kama hospitali na sokoni.

Awali, Meneja TARURA wa Wilaya hiyo Mhandisi Prosper Francis amefafanua kazi zilizofanyika kuwa ni Ujenzi wa kitako cha barabara (Road bed), Tabaka la chini (G15), Tabaka la kati (CM), Tbaka la juu (CRS) pamoja na tabaka la kwanza la lami (Prime-coat) na Ujenzi wa Makalavati 6 yenye kipenyo cha 900 mm.

Katika wakati mwingine Mwenge wa Uhuru umezindua Nyumba ya watumishi wa Zahanati ya Butonga (2 in 1) iliyojengwa kwa zaidi ya Milioni 102 kutoka TASAF na umeweka Jiwe la Msingi shule mpya ya Sekondari ya Isungang’holo iliyojengwa kwa Milioni 584.2 kabla ya kuweka jiwe la msingi Mradi wa Maji wa Bilioni 3.37 katika kijiji cha Sima.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI YA BILIONI 1.3 KWA JESHI LA POLISI

    September 12, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WATUMISHI NCHINI

    September 11, 2025
  • MAJALIWA AAGIZA KUIMARISHWA ZAIDI SEKTA YA UFUATILIAJI, TATHMINI NCHINI

    September 11, 2025
  • NSSF WAFANYA ZIARA YA UWEKEZAJI MWANZA

    September 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.