• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Baraza la Madiwani Kwimba latoa miezi 3 waliokula fedha za Halmashauri wazirejeshe

Posted on: June 22nd, 2022


Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba limetoa miezi mitatu kwa watumishi waliolipwa fedha Tshs Milioni 52 bila vithibitisho, Tshs Milioni 84.1 za Mishahara kwa watumishi waliostaafu na Tshs Milioni 126.5 za Msaada wa Chakula zilizokusanywa na kutotumwa Ofisi ya Waziri Mkuu kinyume na taratibu kurejesha fedha hizo.

Hayo yamerjiri leo Juni 22, 2022 wilayani Kwimba wakati Baraza Maalumu la Madiwani la Halmashauri hiyo lilipokutana kujadili Hoja za Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za Serikali kwa Mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2021.

"Hatukubali kulea uzembe popote ilipo fedha ya umma lazima irudi, hata kama aliyekula amehama akatwe kwenye mshahara wake na kama amestaafu akatwe kwenye pensheni yake ili fedha za Serikali zirudi hapa." amesisitiza Mkuu wa Mkoa Mhe. Mhandisi Robert Gabriel.

Katika wakati mwingine, Mkuu wa Mkoa ameagiza vyombo vya  usalama kuwahoji wataalamu watatu waliohusika kusimamia ujenzi wa jengo la Kantini lililo katika hatua za chini za utekelezaji na kukwama kukamilika kwa zaidi ya miaka 5 hata baada ya kutumia Tshs Milioni 113 kati ya Milioni 160 zilizotengwa.

"Ukimya kwenye mahala ambapo fedha hazitumiki vizuri ni doa kubwa sana ni lazima mpaze sauti kukemea na waliotumia vibaya fedha za umma lazima muwataje na msiruhusu uovu uote mizizi tena," amesema Mkuu wa Mkoa wakati akisisitiza kutolega kwenye kuchukua adhabu kwa wabadhirifu.

"Mkurugenzi lazima uhakikishe kila Mkuu wa Idara anajibu hoja zake na usisite kuchukua hatua kwa yeyote atakayechelewa na mwanasheria kuwa makini naona hauijuwi Halmashauri yako, fuatilia kwa karibu ujue kasi zako vizuri na kufanikisha haya yote lazima muwe na ushirikiano" Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike.

Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Mkoa wa Mwanza, Waziri Shabani amesema Mwaka 2020/21 Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba ilikaguliwa na kupata Hati Inayoridhisha na kuanzia mwaka 2012/13 hadi 2020/2021 Halmashauri hiyo ina jumla ya Hoja 120 ambapo 70 zipo kwenye hatua mbalimbali ya Utekelezaji na 50 zimefungwa.

"Mhe. Mwenyekiti, sababu kubwa ya hoja kutofungwa kwenye Halmashauri hii ni kutokana na Halmashauri kutoweka mkakati thabiti wa kujibu Hoja kikamilifu na Menejimenti kutokua na vielelezo na ushahidi wa kuthibitisha matumizi na malipo mbalimbali yaliyofanyika." Bwana Waziri.


_Mwisho_

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.