Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Benki ya Damu Kanda ya Ziwa yashauriwa kuanza mkakati wa kuwashirikisha Viongozi na Makundi mbalimbali kuhamasisha uchangiaji Damu salama

Posted on: June 14th, 2022

Benki ya Damu salama Kanda ya Ziwa imeshauriwa kuja na mkakati wa kuwashirikisha Viongozi kuanzia ngazi ya Mkoa kushuka chini katika kuhamasisha uchangiaji wa rasilimali hiyo na kufikia malengo ya Mkoa.


Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Wachangia Damu Duniani iliyofanyika leo Mkoani Mwanza, Ngusa amesema zoezi hilo la kuwashirikisha Viongozi na kada mbalimbali litakuja na matokeo chanya kutokana na watu kuhamasika.


"Mkoa wetu kabla ya Sensa ya mwaka huu tuna idadi ya watu Milioni tatu na nimesikia bado tuna changamoto ya kufikia malengo ya damu Mkoa, tushirikiane vizuri na kufika  mahitaji ya chupa 32,400 kwa mwaka zinazohitajika Mkoani."


Ndugu Samike amesema suala lililopo mbele yetu ni kasi na mipango imara ya uhamasishaji ikiwemo kutumia fursa ya mikusanyiko ya watu katika hafla  mbalimbali pia na sehemu za watu kufanyia ibada.


Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dktr. Thomas Rutachunzibwa ameishukuru Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mhe Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuiboresha Benki hiyo ya Damu Kanda ya Ziwa kwa kuleta mashine za kisasa za Damu na mazao yake.

Katika Maadhimisho hayo Katibu Tawala amewakabidhi zawadi ya Majiko ya Gesi wadau waliochangia damu kwa muda mrefu Mkoani Mwanza

Maadhimisho ya Siku ya Wachangia Damu Ulimwenguni hufanyika kila tarehe 14 Juni ikiwa ni heshma ya kutambua mchango wao kwa jamii.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • TUNAHITAJI SULUHISHO KWA VITENDO NAMNA YA KUTEKELEZA MAJUKUMU YA MALEZI : DKT. JINGU

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.