• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Billioni 699 Kujenga daraja Mwanza

Posted on: December 7th, 2019

Bilioni 699 kujenga daraja Mwanza


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Magufuli ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Kigongo- Busisi lenye urefu wa km 3.2 ambalo litagharimu bilioni 699.2 pamoja na barabara unganishi ya kiwango cha lami yenye  urefu wa km 1.66 za kiwango cha lami.

Daraja hilo ambalo linajengwa katika Ziwa Victoria litaunganisha Mikoa ya Mwanza na Geita na kurahisisha usafiri kwa wakazi wa Mikoa hiyo na maeneo yote wanaotumia njia hiyo na ni kubwa nchini na Afrika Mashariki huku likiwa la 6 Afrika.

Akizungumza  wakati wa hafla hiyo ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi huo ambao unatekelezwa na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation(CCECC).

 Mhe.Dkt.Magufuli alisema,fedha za ujenzi wa daraja hilo zinatokana na kodi za wananchi na litakapo kamilika litakuwa chachu katika shughuli za uchumi na uzalishaji ikiwemo kilimo,uvuvi,biashara na Utalii pia ni muhimu katika maendeleo na kujikwamua kiuchumi kwa wakazi wa maeneo hayo.

"Fedha za ujenzi wa mradi huu ni za kwetu wenyewe kupitia makusanyo ya kodi mnazolipa wala hatujaomba msaada mahali popote,hivyo nawataka mtembee kifua mbele kwani Tanzania siyo maskini  bilioni 699.2  karibu bilioni 700 na bado bilioni 300 ifike tirioni 1,tukiamua tunaweza,daraja hili ni muhimu kwa maisha ya wanamisungwi,Sengerema  Tanzania na nchi za jirani kwani kuna watu  ambao wamepoteza maisha  hasa kipindi cha nyuma  kutokana  na kutumia mitubwi kuvuka wakati kivuko kilipopata hitilafu na wengine wanapochelewa kivuko kutoka Sengerema na maeneo mengine wakiwa  wanaenda hospitali ya Bugando kwa ajili ya kupata matibabu," alisema Mhe. Dkt.Magufuli.

Hata hivyo alisema,mradi huu ni muhimu katika maendeleo ya  Misungwi na Sengerema endapo wakazi wake watautumia vizuri,hivyo aliwahimiza vijana wa maeneo hayo kujitokeza kufanya kazi na wasikubali watu kutoka maeneo mengine ndiyo wafanye kazi katika mradi huo huku mama lishe na wananchi kwa ujumla wakiutumia kwa kufanya biashara.

Mhe.Dkt.Magufuli alisema,wale wote ambao mradi umewafuata watalipwa fidia kwani zaidi ya bilioni 3.145  zimetengwa kwa ajili hiyo na watakao lipwa ni wale tu wanaohusika na eneo la ardhi siyo majini.

"Uongozi wa Mkoa wa Mwanza hakikisheni wananchi wa maeneo yanayozunguka mradi  huu mnawapa  kipaumbele cha ajira wakati ujenzi wa daraja hili,na mtakaopewa nafasi fanyeni kazi na siyo kuiba vifaa,ni wasihi  watanzania kulipa kodi kwani tukipata fedha zetu tunaweza kufanya mambo yetu wenyewe," alisema Dkt.Magufuli.

Aidha aliwataka,wakandarasi hao waharakishe mradi huo haraka  ikiwezekana wafanye kazi  usiku na mchana ili  ukamilike kwa wakati au kabla ya muda kwani ni muhimu sana kwa  nchi na maisha ya watanzania.

Kwa upande wake Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe.Mhandisi Isaack Kamwele alisema,mradi huo utatumia miezi 48 ( miaka 4) kukamilika ambapo barabara unganishi ya daraja hilo  ni sehemu ya barabara kuu ya usagara  ambayo inaunganisha Mikoa ya Kanda ya Ziwa na nchi jirani kama Uganda,Congo na Rwanda.

Mhandisi Kamwele alisema,daraja hilo litasaidia kuondoa kero ya wananchi ya kutumia muda mrefu kusafirisha mizigo na abiria wakati wa kuvuka  eneo hilo la Ziwa Victoria kati ya Kigongo -Busisi pia kuimarisha usalama huku uboreshaji na ujenzi wa miundombinu nchini ni sehemu ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2015 na maono yake ya mwaka 2025.

Naye Mtendaji wa Mkuu wa TANROAD Mhandisi Patrick Mfugale alisema,kuanzia wiki ijayo wataanza kutoa fidia kwa  wananchi ambao wamepitiwa na mradi huo ambapo ujenzi wake utakuwa bora ambao utadumu kwa miaka mia ijayo.

Aidha mmoja wa wananchi wa Misungwi Neema Emmanuel alisema,endapo daraja hilo litakamilika litawasaidia katika kufanya shughuli zao za kiuchumi na kusafiri kutoka eneo moja kwenda jingine kwani anaamini pia kutakua na uanzishwaji wa daladala ambao utakuwa na gharama nafuu na kuchukua muda mchache pamoja na kuwa na uhakika wa kusafiri wakati wote kwa kuvuka eneo hilo la maji tofauti na sasa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.