• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BIMA YA AFYA KWA WOTE NI NGUZO YA MAENDELEO – RC MTANDA

Posted on: February 10th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewahimiza wananchi wa mkoa huo kuchangamkia mpango wa Bima ya Afya kwa Wote ili kujihakikishia huduma bora za afya wakati wote.

Ameyasema hayo alipokuwa akikagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya Kayenze, ambapo amesisitiza umuhimu wa kuwa na maandalizi ya kiafya mapema.

RC Mtanda amesema mpango huo unamlazimu kila mwananchi kuchangia kiasi cha shilingi laki moja na elfu hamsini (150,000) kwa mwaka, kwa familia yenye hadi watu sita. Amesema gharama hiyo ni ndogo ukilinganisha na faida kubwa zinazopatikana kupitia bima hiyo.

Ameeleza kuwa kifurushi cha bima hiyo kinajumuisha huduma zaidi ya 372 za afya, jambo linalowezesha familia kupata matibabu mbalimbali bila mzigo mkubwa wa kifedha wakati wa dharura.

Mkuu wa Mkoa amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kujiunga na bima hiyo pindi fursa itakapopatikana, akisisitiza kuwa afya ni msingi wa maendeleo ya mtu binafsi na jamii kwa ujumla.

Ameongeza kuwa mahitaji muhimu kwa binadamu ni chakula, afya na makazi, hivyo ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anajilinda kiafya kwa kukata bima ya afya kwa ajili ya ustawi wa maisha yake na familia yake.

Akijibu hoja ya barabara iliyowasilishwa na Diwani wa kata hiyo, Mkuu wa Mkoa amesema kuwa baada ya muda mfupi ujao barabara ya Kayenze itaanza kutengenezwa ili kuboresha miundombinu ya usafiri katika eneo hilo. Aidha, amegusia suala la umeme kwa kueleza kuwa maboresho makubwa yanaendelea kufanyika, na mara baada ya kukamilika hakutakuwa tena na adha ya kukatika-katika kwa huduma ya umeme kwa wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AZINDUA SHULE YA SEKONDARI BUMYENGEJA KWIMBA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AZINDUA NYUMBA YA WATUMISHI KITUO CHA AFYA BUDUSHI, ATOA WITO KUJIUNGA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.