• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BLUE VICTORIA YAZINDUA MIRADI YA KISASA KULINDA MAZINGIRA YA ZIWA VICTORIA

Posted on: October 24th, 2025

Shirika lisilo la kiserikali la Blue Victoria limezindua miradi miwili bunifu inayolenga kulinda mazingira ya Ziwa Victoria, ikiwemo mradi wa ufuatiliaji wa vifereji kwa kutumia teknolojia ya kisasa na mradi wa kuondoa nyavu zilizotelekezwa majini, maarufu kama Ghost Nets.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa ufuatiliaji wa mifereji kwa kutumia teknolojia ya kisasa ambao utasaidia kubaini vyanzo vya uchafuzi vinavyoingia ziwani, na mradi wa kuondoa nyavu zilizotelekezwa (Ghost Nets) ambazo zimekuwa tishio kwa samaki, wavuvi na bioanuai ya ziwa hilo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Kaimu Katibu Tawala anaeshughulikia Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Mwanza Bw. Peter Kasele amelipongeza shirika la Blue Victoria kwa ubunifu na mchango wake katika juhudi za kulinda mazingira, akisema miradi hiyo ni mfano wa ushirikiano mzuri kati ya sekta binafsi na serikali katika kutatua changamoto za kimazingira.

Bw. Kasele amesema miradi hiyo imekuja ndani ya muda muafaka kwakua kiferezi ni tukio la kiasili ambalo limekua changamoto ambayo inasababisha samaki kufa kwa wingi hali ambayo inahatarisha shughuli za uvuvi.

"Matukio ya kiferezi huleta taharuki na hasara kwa wavuvi na wafugaji wa samaki na madhara kwa mazingira ya ziwa kwakua samaki wanakufa". Amesema Bw. Kasele.


Aidha, ameongeza kuwa jitihada hizo za sekta binafsi kuiunga mkono serikali inachangia kuimarisha uvuvi endelevu, uhifadhi wa biyoanuia na matumizi bora ya teknolojia katika kusimamia mazingira ya asili.

Naye, Mfawidhi wa Uvuvi Kanda ya Ziwa Victoria amesema anawashukuru wadau wa maendeleo kwa pamoja kwa kuziunga mkono jitihada za Serikali na kushirikiana nayo katika kuikuza sekta ya uvuvi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Blue Victoria Festus Massaho amesema teknolojia wanayoizindua inaenda kutatua changamoto zitakazojitokeza katika shughuli za uvuvi na maisha ya viumbe maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AIPONGEZA OFISI YA WAZIRI MKUU KUANZISHA KAMATI ZA MAAFA ZA MIKOA

    November 18, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA WATAKWIMU KUTOA TAKWIMU SAHIHI KUCHAGIZA MAENDELEO

    November 18, 2025
  • RAS MWANZA AONGOZA WAOMBOLEZAJI MAZISHI YA ALIYEKUWA MTUMISHI WA MWAUWASA

    November 14, 2025
  • MWANZA YASHIRIKI MAFUNZO KUKUZA USAWA WA KIJINSIA NCHINI MKOANI MOROGORO

    November 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.