• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Bodaboda Mwanza wachangia damu majelui wa ajali Morogoro

Posted on: August 15th, 2019


Umoja wa Waendesha pikipiki Mkoa wa Mwanza (Bodaboda) wamejitokeza kwa wingi jijini hapa kuwachangia damu majeruhi wa ajali ya moto iliyotokea hivi karibuni mkoani Morogoro na kuua watu zaidi ya 90 na kujeruhi zaidi ya watu 40.

Akizungumza na wandishi wa habari mara baada ya kuchangia damu, Mwenyekiti wa Chama cha Bodaboda Mkoa wa Mwanza Jerald Nyembe alisema wao kama bodaboda wameguswa na tukio la ajali lililotokea mkoani Morogoro na hivyo wakaona ni vyema kuungana na watanzania wengine nchini ili waweze kuwachangia ndugu ambao ni majeruhi wa ajali hiyo.

“Tumeitikia wito wa Serikali hasa wa Rais wetu mpendwa Dkt. John Magufuli wa kuwachangia ndugu zetu damu, ambao kwa sasa wana uhitaji mkubwa,” alisema.

Kwa upande wao, Atanas Lugela na Richard George ambao ni boda boda wanaofanyia shughuli zao jijini Mwanza, walisema tukio la ajali iliyojeruhi na kusababisha watu zaidi ya 700 limewagusa sana na hivyo waliona ni vyema wajitokeze kuchangia damu, ambayo licha ya kusaidia majeruhi ya ajali wa mkoa wa Morogoro, itayasaidia makundi mengine katika jamii, wakiwemo akinamama wajawazito, watoto na majeruhi wengine nchini ambao wana uhitaji mkubwa wa damu.

“Nimeguswa na tukio la Morogoro, na nina hofu ya kesho na ndiyo maana nimejitokeza kuchangia damu, naomba watu wengine nchini nao washiriki kuchangia damu,” alisema.

Kwa upande wake Mratibu wa Huduma za Maabara na Damu Salama Mkoa wa Mwanza Juma Shigella licha ya kuwapongeza bodaboda wa jijini Mwanza kuitikia mwito wa serikali na kujitokeza kuchangia damu, alisema mahitaji ya damu kwa mkoa kwa siku ni chupa 80 kwa siku na kwa mwezi ni chupa 2,400.

Alisema hata hivyo mkoa una uwezo wa kukusanya asilimia 60 tu ya mahitaji na hivyo kuwa na upungufu wa asilimia 40 ya chupa za damu zinazohitajika kimkoa.

Alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella ambaye kupitia kwake, mkoa uliweza kukusanya zaidi ya chupa 4000 za damu wakati wa maadhimisho ya Siku ya Damu Salama ambayo kitaifa yalifanyika mkoani Mwanza.

“Nawaomba watu wajenge utamaduni wa kujitokeza  kuchangia damu, kwa sababu duniani kote hakuna kiwanda cha kuteng’eneza damu, na damu inapopatikana inawasaidia watu wote katika jamii,” alisema.

Akizungumza kwenye hafla hiyo ya kuchangia damu, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza Jumanne Muliro aliwapongeza boda boda hao kwa uamuzi wao wa kujitokeza kuwachangia damu ndugu zao ambao ni majeruhi wa ajali iliyotokea mkoani Morogoro na kwamba wameonyesha kitendo cha ubinadamu na kuwaomba watu, vikundi, asasi na taasisi za umma kuiga mfano wao.

“Zoezi la uchangiaji damu halizingatii chama wala dini, au kabila, nawashukuru sana kwa jambo hilo mlilofanya,” alisema.

Alisema  utambuzi uliofanywa na serikali wa kuitambua na kuirasimisha sekta ya bodaboda nchini umepunguza ajali na kuongeza ajira kwa vijana ambapo pia aliwaomba viongozi wa dini na kisiasa kuiga mfano ulionyeshwa na bodaboda hao kwa kujitokeza kuchangia damu.

“ Niwaombe muendelee kuzingatia kanuni na sheria za usalama barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu na tushirikiane kwa pamoja kuwakemea na kuwabaini watu wanaotumia bodaboda kufanya uhalifu,” alisema Kamanda Muliro.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.