• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

BODABODA MWANZA WALAANI MAANDAMANO YA CHADEMA YA FEBRUARI 15

Posted on: February 14th, 2024

BODABODA MWANZA WALAANI MAANDAMANO YA CHADEMA YA FEBRUARI 15


*Wasema wanajivunia kazi yao kwenye utulivu na amani*


*Wasema wanaomboleza msiba wa aliyekuwa Waziri Mkuu*


 *Walaani kiongozi wa CHADEMA kuita bodaboda ni kazi ya laana*


Waendesha Pikipiki (Bodaboda) Jijini Mwanza wamelaani maandamano yanayoratibiwa na Chama cha Demekrasia na Maendeleo (CHADEMA) yanayotarajiwa kufanyika Mkoani Mwanza mnamo tarehe 15/02/2024 huku wakibainisha kuwa hayana afya kwa Taifa.


Wamesema, hawako tayari kuandamana badala yake wataendelea kushiriki kikamilifu maombolezo ya siku 5 yaliyotangazwa na Rais Samia Suluhu Hassan kufuatia kifo cha aliyekua Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Edward Lowassa na si mambo mengine ambayo hayana uungwana.

Makamu Mwenyekiti wa Bodaboda Mwanza John Razaro amesisitiza kwa kusema kuwa hawawezi kuandamana kutokana na msiba wa kiongozi ambaye alikuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa.

Vilevile, wamesema kwa sauti moja wanalaani vikali maandamano hayo na kuahidi kutojihusisha nayo kabisa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo pia kauli iliyotolewa na kiongozi wa upinzani siku za nyuma ikieleza kuwa kazi ya bodaboda ni kazi ya laana.

"Kuna kiongozi aliwahi kusema kuwa bodaboda ni kazi ya laana hivyo haifai kufanywa na binadamu, kauli hii ilituumiza sana na hatuwezi kuungana na watu ambao wameona kazi yetu ni ya laana ikiwa kazi hii inasaidia maisha ya familia zetu’’ , Lazaro.

Naye, Mororo Daniel ambaye ni mmoja wa wanachama wa umoja wa bodaboda Buhongwa ameeleza kuwa haoni tija ya kujiingiza katika maandamano hayo kwani Serikali imekuwa ikifanya mambo mengi mazuri ambayo wananchi wamekuwa wakinufaika nayo ikiwemo ujenzi wa hospitali, shule pamoja na miundombinu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BONDE LA ZIWA VICTORIA KWA KUELIMISHA UMMA

    May 13, 2025
  • RC MTANDA ASISITIZA UIMARISHWAJI WA UMOJA NA MSHIKAMANO

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.