• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Daima tupo Tayari - Mongella

Posted on: March 23rd, 2020

Mwezi Novemba na Desemba 2019 pengine ni kati ya vipindi ambavyo mkoa wa Mwanza umeshuhudia na kupokea ugeni mkubwa Kitaifa na Kimataifa.

Ni kipindi hicho ndipo maadhimishi ya wiki ya siku ya Ukimwi yalipofanyika jijini Mwanza ikiwaleta pamoja viongozi wa Kitaifa na Kimataifa.

Kitaifa walikuwepo Mawaziri, Watendaji wakuu wa taasisi zinazohusika na mapambano dhidi ya Ukimwi, wasanii pamoja na wawakilishi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wanaohusika na masuala ya Ukimwi (UNAIDS), wanawake (UN WOMEN na kazi (ILO).

Kilele cha maadhimisho hayo vilivyofanyika katika viwanja vya Rock city Mall vilishirikisha watu kutoka makundi mbalimbali ya kijamii wakiwemo vijana na wazee wake kwa waume.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai ni kati ya viongozi wa Kitaifa waliofika Mwanza katika wiki ya siku ya Ukimwi kwa ajili ya kuhudhuria kongamano maalum lililoandaliwa na Kamati ya kupambana na Kifua Kikuu (TB).

Kongamano hilo lilijumuisha wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini na wastaafu wakiongozwa na Waziri Mkuu mstaafu, Mizengo Pinda.

Orodha ya viongozi wa Kitaifa waliofika Mwanza kuanzia maadhimisho ya Ukimwi pia wamo Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na wenye ulemavu) Jenista Mhagama na Katibu wa Baraza la Ulama Taifa Sheikh Hassan Said Chizenga.

Pia walikuwemo Makamu wa Pili wa Mwenyekiti wa Baraza la Makanisa Tanzania (CCT) Jacob Chimeledy na Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge walio kwenye mapambano TB nje ya Bunge, Osca Mkasa.

Latola ngazi ya Kimataifa,

Mwanza pia imewapokea wawakilishi wakazi wa mashirika na taasisi za Umoja wa Mataifa walioongozwa na Mwakilishi mkazi wa UN AIDS, Dk Leo Zekeng.

Maadhimisho ya siku ya Ukimwi yameambatana na maadhimisho mengine ya siku 16 ya kupiga vita vitendo vya ukatili na unyanyasaji kujinsia dhidi ya wanawake na watoto ambapo hoja ya kuwepo pete tegesha za uchumba miongoni mwa wanafunzi wa taasisi za elimu ya juu iliibuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Kivulini, Yassin Ally.

Taarifa za pete tegesha za uchumba na ndoa za kuwalaghai wanafunzi wa kike zimeigutusha Serikali ambayo kupitia Waziri Mhagama imetangaza kuitisha kikao cha wadau wote ifikapo Januari, 2020 kujadili na kutafutia ufumbuzi suala hilo.

Akihutubia kilele cha siku ya Ukimwi katika viwanja vya Rock city Mall kwa niaba ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Waziri Mhagama akautaarifu umma kuwa kikao hicho kitaandaliwa kupitia uratibu wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Wazira ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.