• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

Posted on: January 28th, 2026

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza imefanya kikao kazi na viongozi na watendaji wa Halmashauri za Mkoa huo kwa lengo la kuwajengea uwezo kuhusu ujio wa Daftari la Makazi na Bima ya Afya kwa Wote.

Akifungua kikao hicho, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amesema Daftari la Makazi linalenga kuwasajili wananchi wote kwa ngazi ya kaya ili kurahisisha utambuzi na upatikanaji wa huduma za kijamii.

Amesema Wenyeviti wa Mitaa na Vijiji watakuwa wahusika wakuu wa kusimamia madaftari hayo, huku wananchi wakitakiwa kuhakikisha wanajisajili.

Aidha amesisitiza kuwa ni wakati sasa kwa viongozi na watendaji kwenda kutoa elimu kwa wananchi.

Ndugu Balandya ameongeza kuwa Bima ya Afya kwa Wote tayari imezinduliwa na Waziri wa Afya na kwamba juhudi zinaendelea kuhakikisha wananchi wanapata elimu kuhusu huduma 372 zinazopatikana kuanzia ngazi ya zahanati hadi mkoa kupitia kitita cha jamii.

Kwa upande wake, Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Mkoa wa Mwanza Bw. Jarlath Mushashu amesema Mkoa ulizindua rasmi uhamasishaji wa elimu ya bima tarehe 17 Desemba, 2025 ili kila mwananchi apate uelewa wa mfuko huo.

Ameeleza kuwa Bima ya Afya kwa Wote itasogeza huduma karibu na wananchi na kuwezesha usajili wa bima kwa makundi mbalimbali ikiwemo kaya na mashirika huku mfumo wa huduma ukiwa ni wa kulipia kabla ya kupata huduma.

Amefafanua kuwa kaya yenye watu kuanzia mmoja hadi sita italipia Tshs. 150,000 kwa mwaka, ambapo wanufaika watasajiliwa kwenye mfumo maalumu unaosomana na mifumo mingine ya Serikali.

Kikao kazi hicho kilichowahusisha Mameya, Wenyeviti, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Maafisa Mipango, Utumishi na Waweka Hazina, pia kimejumuisha mafunzo ya Mpango wa Ufadhili Mbadala unaoratibiwa na Wizara ya Fedha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

    January 29, 2026
  • HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • TRA MWANZA YATOA MAFUNZO YA MFUMO JUMUISHI WA KODI ZA NDANI KWA WAFANYABIASHARA

    January 28, 2026
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI WA WIZARA YA ULINZI NA JKT MWANZA

    January 28, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.