• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DKT BITEKO AONGOZA KONGAMANO LA KIKANDA DIRA YA TAIFA 2050 MWANZA

Posted on: July 20th, 2024

DKT BITEKO AONGOZA KONGAMANO LA KIKANDA DIRA YA TAIFA 2050 MWANZA


Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Julai 20, 2024 ameongoza kongamano la kwanza kuhusu maandalizi ya Dira ya Taifa ya maendeleo 2050 lililofanyika Mkoani Mwanza kwenye ukumbi wa Kwatunza Beach Resort.

Akizindua kongamano hilo pamoja na taarifa ya maendeleo ya watu Dkt. Biteko ametoa wito kwa wananchi kushiriki kikamilifu kutoa maoni ili kumiliki dira itakayofikiwa, kuwahusisha moja kwa moja makundi ya kiuchumi pamoja na kusaidia kukubaliana na changamoto zilizobainika katika utekelezaji wa dira ya sasa.

Aidha, amesema ukuaji na muendelezo wa mageuzi kiuchumi ndani ya nchi yameendelea kuimarika ukilinganisha na tulikotoka kwa wastani wa asilimia 6.1 kutoka mwaka 2000 hadi 2021 na sasa Taifa lipo kwenye wakati muhimu wa kuandaa mpango kabambe wa kuamua tunataka kuishi vipi miaka 25 ijayo.

"Duniani kwa sasa kuna matishio ya maendeleo kama mabadiliko ya tabia nchi, mabadiliko ya kiteknolojia, kidemografia na machafuko ya kisiasa na hatuna budi kuyakwepa na kuweka juhudi na bidii kwenye uandaaji wa mipango thabiti ya kukua kiuchumi". Mhe. Dkt. Biteko.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema mkoa huo wenye watu zaidi ya Milioni 3.6 unachangia pato la taifa kwa Tshs. Trilioni 12.2 huku ukiwa ni mkoa wa pili kwa uchangiaji kwa asilimia 7.1 ukitanguliwa na Dar es Salaam pekee.

 

"Mkoa wetu umejiimarisha kwenye sekta za viwanda, ujenzi, kilimo, maji, utalii, ufugaji na uvuvi na tunaendelea kuzibaini na kutatua changamoto ili tuendelee kuimarika kwenye uchangiaji wa pato la Taifa na ukuzaji wa uchumi wa nchi." Amefafanua.

Aidha, amemshukuru Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi kwenye miradi ya kimkakati ya maendeleo inayotekelezwa mkoani humo kama ujenzi wa daraja la Kigongo-Busisi (Bilioni 716), Reli ya Kisasa (SGR), Vivuko vipya (Bilioni 28),  Soko la kisasa la mjini kati (Bilioni 23), mradi wa chanzo cha maji Butimba (Bilioni 79) pamoja na usambazaji (Bilioni 400) na Meli ya Kisasa kwa bilioni 123

Kongamano hilo lililowakutanisha wadau kutoka Mikoa ya Mwanza, Geita, Kagera, Shinyanga, Mara na Simiyu limechagizwa na kaulimbiu isemayo "Tanzania Tuitakayo 2050 Dira yako, Dira Yetu".

Aidha wananchi wanaweza kutoa maoni yao kupitia *152*00# bila malipo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.