• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

Posted on: January 10th, 2026

Mashabiki wahimizwa kudumisha amani, mshikamano na heshima

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mechi ya kirafiki itakayozikutanisha mashabiki wa klabu za Simba na Pamba, itakayochezwa Januari 12, 2026 katika Uwanja wa Nyamagana, Jijini Mwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Januari 10, 2026, Mratibu wa mashindano hayo, Bw. Mohammed Bitegeko amesema mechi hiyo imeandaliwa mahsusi kuwaleta pamoja mashabiki wa klabu hizo mbili zenye historia na ushawishi mkubwa katika soka la Mwanza na Tanzania.

Amefafanua kuwa lengo kuu la pambano hilo si ushindani wa kawaida bali ni kuimarisha umoja, mshikamano na upendo miongoni mwa mashabiki wa Simba na Pamba, huku ikionyesha wazi kuwa mpira wa miguu ni nyenzo ya amani na maelewano.

Aidha, amesema mechi hiyo inalenga kukuza michezo na utalii wa michezo mkoani Mwanza, sambamba na juhudi za serikali katika kutumia michezo kama chachu ya maendeleo ya jamii.

Kwa mujibu wa Mratibu huyo, mechi itasimamiwa na waamuzi wa soka wenye viwango vya FIFA ili kulinda hadhi ya mchezo, kuzingatia sheria na kuhakikisha usalama wa wachezaji pamoja na mashabiki.

Katibu wa Mashabiki wa Simba Mkoa wa Mwanza Bw. Philbert Kabago amesema Simba itawakilishwa pia na wachezaji wake wa zamani wanaoishi mkoani Mwanza, akisisitiza kuwa maandalizi yako katika hatua za mwisho.

Kwa upande wake, Afisa Habari wa Pamba Jiji, Moses William amesema Pamba iko tayari kwa pambano hilo la kirafiki, huku akibainisha kuwa klabu hiyo pia itashirikisha wachezaji wake wakongwe waliowahi kuitumikia timu hiyo.

Kamati ya maandalizi imewahimiza mashabiki wa pande zote mbili kujitokeza kwa wingi, huku wakizingatia amani, nidhamu, heshima na upendo siku ya mechi.

Mechi hiyo inatarajiwa kuwa mfano wa kuigwa, ikionyesha kuwa Simba na Pamba wanaweza kushindana kwa heshima na kuishi kwa amani kama ndugu.

Simba na Pamba – Ushindani wa Kirafiki, Umoja na Amani ya Kudumu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MRADI WA UMWAGILIAJI IBANDA–IGAKA WA BILIONI 35 HAUTASIMAMA – SILINDE

    January 10, 2026
  • RC MTANDA MGENI RASMI MECHI YA KIRAFIKI SIMBA VS PAMBA MWANZA

    January 10, 2026
  • BODI YA BARABARA MWANZA YATAKIWA KUSIMAMIA UBORA NA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA

    January 08, 2026
  • MHE. KUNDO KUKAGUA MIRADI YA MAJI MWANZA KWA SIKU TATU

    January 07, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.