• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Dkt.Mpango aagiza uadilifu utekelezaji miradi ya maendeleo

Posted on: April 11th, 2023


Makamu wa Rais Mhe.Dk t. Philip Isdor Mpango ameiagiza Wizara ya Ofisi ya RaisTawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( OR- TAMISEMI) kuona namna ya kuongeza mabweni katika shule sita za Sekondari zilizopo  Jimbo la Kwimba Mkoani Mwanza ili  kuwaondolea changamoto ya umbali na vishawishi kutoka kwa wanaume wanafunzi wa kike.

Pia amewaasa wananchi kutunza miundombinu ya miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ili idumu na kuwahudumia kwa muda mrefu kwani fedha zinazotumika kuijenga ni zao wote kwa kuwa wanalipa kodi.

Mhe.Dkt.Mpango ametoa maagizo hayo leo Aprili 11,2023 wakati akiwasalimia wananchi wa Kata  ya Hungumalwa Wilaya ya Kwimba Mkoa wa Mwanza akiwa katika ziara ya kikazi mkoani humo.

Mhe.Dkt.Mpango alitoa agizo kwa TAMISEMI baada ya Mbunge wa Jimbo la Kwimba Atlaf Mansoor kuiomba Serikali kujenga mabweni na maabara   kwenye shule  sita zilizopo Kata  ya  Hungumalwa ili wanafunzi waweze kulala shuleni waepuka vishawishi mbalimbali vinavyowasababishia kushindwa kuhitimu masomo yao na  kutimiza ndoto zao.

Mhe.Dkt.Mpango aliwasihi wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao shule ili wasome na kupata elimu  na utaalamu katika sekta mbalimbali kwa faida ya taifa.

"Ili kujenga taifa la kesho lenye vijana na watu wenye uwezo mkubwa wa kufikiri   lazima watoto wetu waende shule pia naomba taasisi binafsi, za serikali na wadau wote wa maendeleo ifundisheni jamii kuhusu  umuhimu wa  lishe bora hasa kwa watoto na akina mama wajawazito,"amesema.

Akizungumzia umuhimu wa wananchi kutunza miundombinu, Mhe.Dkt. Mpango amesema serikali imetoa fedha nyingi  katika mikoa yote nchi nzima kwa ajili ya miradi  ya  maendeleo  ili iwanufaishe  wananchi wake na kuwaondolea changamoto mbalimbali zinazowakabili.

"Viongozi na wananchi wote mshiriki kikamilifu kwenye miradi hiyo, wananchi muitunze na viongozi wa umma muwe waadilifu wa fedha hizo za umma zinazotumika kujenga miradi hiyo  ili  ijengwe  kwa ubora ikiwa na  thamani halisi ya fedha zilizotengwa,"amesema Mhe. Dkt.Mpango.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima akizungumzia hali ya utoro mkoani humo  amesema   hadi mwishoni mwa Februari mwaka huu  2023 baadhi ya wanafunzi walikuwa

 bado hawajaripoti shuleni lakini uongozi wa mkoa  kwa kushirikiana na halmashauri husika wanaendelea kufanya jitihada mbalimbali ili kutatua  changamoto hiyo .

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.