• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Dkt.Mpango azitaka Taasisi za Fedha nchini kushusha riba za Mikopo

Posted on: November 24th, 2022

*Dkt.Mpango azitaka Taasisi za kifedha nchini kushusha riba za Mikopo*


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amezitaka Taasisi za kifedha nchini kufanya uchambuzi wa kitaalamu ili riba za ukopeshaji zishuke kwa lengo Watanzania wengi wanufaike na huduma hiyo ambayo ni chachu ya maendeleo ya Taifa.

Akifungua rasmi wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa leo Mkoani Mwanza, Dkt Mpango amesema Serikali imekuwa ikiendelea kuhimiza Taasisi hizo kupunguza riba lakini kumekuwa na muitikio hafifu hali ambayo inawanyima walio wengi kupiga hatua kiuchumi.

"Ukitazama maeneo kama vijijini ni asilimia 8.6 tu ndiyo wanapata huduma za kifedha, hiyo bado ni ndogo sana ukizingatia huko ndiko eneo kubwa la uzalishaji wa kilimo", amesema Makamu wa Rais.

Amesema, baada ya zoezi la Sensa limeonesha sasa tumefikia idadi ya watu Milioni 61.74 kundi kubwa likiwa ni vijana amezitaka Taasisi za kifedha nchini kubuni mkakati wa kulifikia soko hilo ambalo ni nguvu kazi ya Taifa.

"Mhe Rais Samia Suluhu Hassan ameshatoa maelekezo kuhakikisha kundi la Vijana linawekewa mpango maalum ili liweze kujiajiri ,naimani kupitia wiki hii mmewagusa kwa kuwapatia elimu ya fedha na mkakati wa kuwainua kiuchumi"amesisitiza Dkt.Mpango.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Meja Jenerali Suleiman Mzee ameishukuru Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuleta wiki hiyo kutokana na Mkoa huo upo Kimkakati kwa kupakana na nchi jirani na kuwa kitovu cha biashara.

"Jumla ya Taasisi 90 za kutoa huduma za kifedha zimepewa leseni na Saccos 64 pia zimepatiwa leseni,hali hii itaongeza wigo kwa wananchi kunufaika katika shughuli zao za kujiletea maendeleo" amesema Kaimu Mkuu huyo wa Mkoa.

Akizungumzia malengo ya wiki hiyo Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Hamad Chande amesema huu ni mwaka wa pili tangu wameanza kufanya na kumekuwa na muitikio chanya tangu Serikali imefanya maboresha katika Sekta za kifedha nchini.

"Mhe Makamu wa Rais maboresho hayo ni pamoja na kuweka sera rafiki ili sekta ya kifedha iwafikie wengi pia kumekuwepo na Mamlaka nyingi za usimamizi wa fedha zenya majukumu ya kuhakikisha huduma hii inafanyika kitaalamu ili malengo yatimie ya asilimia 80 hadi mwaka 2025 wawe na elimu kuhusiana na huduma za kifedha"Mhe.Naibu Waziri.

Wiki ya Huduma za Kifedha Kitaifa inaandaliwa na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kushirikiana na wadau wake, Mwanza wakiwa wenyeji wakitanguliwa na Mkoa wa Dar-es-Salaam kulikofanyika mwaka jana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.