• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Elimu ya maadili yatolewa Mwanza kwa Viongozi

Posted on: December 10th, 2020

Viongozi wa Serikali na wadau mbalimbali watakiwa kuishi kwa maadili na uadilifu ili kujenga nguzo bora yenye  kuleta tija katika kukuza na kuchochea maendeleo ya nchi.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella alipokuwa  Akifungua kikao kazi cha maadhimisho ya siku ya maadili na haki za binadamu iliyofanyika Jijini Mwanza, amesema kufuata maadili siyo matukio bali inapaswa kufanywa kwa maisha ya kila siku .

" Mfano mtu anakunywa hakatazwi lakini kuna sehemu kiongozi kama Mkuu wa Mkoa hupaswi kuwa zaidi ya masaa mawili lakini unakuta mtu anakunywa mpaka anashindana kuzungusha laundi ukiulizwa unasema nalinda kura au naamasisha wananchi huku ndipo wapo wengi tuache tabia hizo na tujidhibiti na kufanya Kazi ipasavyo kama anavyofanya Rais Magufuli ili kuleta maendeleo kwa kasi" amesema Mongella.

Naye Katibu Msaidizi wa maadili ya Viongozi wa Umma Kanda ya Ziwa Godson Kweka akiwasilisha mada ya maadili amesema  madhara ambayo yanawezwa kuletwa na kiongozi asiyekuwa na maadali ni makubwa hivyo yawapasa kutambua uongozi ni dhamana ya kuhakikisha unatekeleza majukumu uliopatiwa kikamilifu.

" Kauli mbiu ya mwaka huu ni "Uzingatiaji wa ahadi ya uadilifu kwa viongozi na watumishi wa ustawi wa utawala bora na haki za binadamu", watumishi mtambue nafasi mlizopewa ni kwa maslahi ya umma na kuwatumikia wananchi na kutotumia nafasi hiyo kwenda kinyume na maadali wengine wanatumia nafasi zao vibaya kwa kutowajibika,kujihusisha, kuwanufaisha marafiki, ndugu na siyo jamii " amesema Kweka.

Naye Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Mwanza Emmanuel Stenga akiwasilisha hali ya rushwa kwa mkoa amesema wamekuwa wakitekeleza majukumu ya kisheria ya kuzuia ,kuelimisha na kupambana na rushwa na kutekeleza maagizo ya Rais Magufuli ya kutetea wanyonge dhidi ya vitendo vya dhuluma na visivyo vya kiutu.

Ameongeza kwa kipindi cha Julai 2015 Hadi Juni  2020 kwa dawati la uchunguzi pekee TAKUKURU Mkoa wa Mwanza imekamilisha uchunguzi wa majalada 209,kesi 125 zimefikishwa mahakamani, kesi 62 washtakiwa wametiwa hatiani, kesi 49 washtakiwa wameachiwa huku majalada 30 ya watumishi yaliyokuwa yakichunguzwa wamechukuliwa hatua za kinidhamu.

"Kwa kipindi cha mwaka mmoja wa fedha uliopita,Julai 2019 hadi Juni 2020 TAKUKURU mkoani hapa imepokea taarifa 831 , taarifa hizi zinahusisha makosa ya rushwa,makosa mengine ya jinai ambayo siyo rushwa ,vitendo vya dhuluma, ucheleweshaji ama kunyimwa huduma na haki" anaeleza Stenga.

Kwa upande wake Afisa Mfawidhi Afisi ya Kanda ya Mwanza Tume ya Haki za Binadamu na Utawala bora Albert Kakengi amesema dhana ya utawala bora ni pana ambayo inasisitizwa duniani kote kuwa ndiyo msingi utaofikia malengo ya milenia, pia ukuaji wa uchumi utasaidia kupunguza umaskini wa kipato na kuimarisha ubora wa maisha na ustawi wa Jamii na isipozingatiwa itachukua muda mrefu kuyafanya hayo.

Dkt.Jacob Mutash ambaye ni Mchungaji wa kanisa la EAGT Kiloleli na Sheikh wa Mkoa wa Mwanza Hassan Kabeki akizungumzia suala la maadili na uadilifu walisema viongozi wanapaswa kuwa na hofu ya Mungu na kuyazingatia kwa kutenda yale yaliomema na kuwa na bidii ya kutenda kazi ili kuijenga nchi yenye kuleta nuru kwa watu wote.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.