• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Halmashauri kuu Yahamasisha kasi ya maendeleo

Posted on: January 24th, 2020


Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya  Chama Cha Mapinduzi  Taifa (NEC)  wamefanya ziara ya kukagua  miradi  yote  ya kimkakati katika Mkoa wa Mwanza na kusema kwamba  kama kusingekuwapo na katiba, Mhe. Rais  Dk.John Magufuli angetakiwa kuendelea kuongoza Tanzania hadi pale atakapoona inamfaa kustaafu mwenyewe.


Pia baadhi ya wajumbe  wa NEC walisema itashangaza  endapo itatotokea kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) atajitokeza kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi ujao wa 2020 kwani itakuwa ni ishara ya kumkwamisha Rais Dk. Magufuli asitimize malengo yake.


Ziara hiyo iliyoongozwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa, Mhe. Humphery Polepole pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella ilianzia  ukaguzi wa daraja la juu la watembea kwa miguu la Furahisha,  upanuzi wa barabara Makongoro  inayoanzia  eneo la Ghana hadi  uwanja wa ndege wa Mwanza.


Miradi mingine iliyotembelewa ni  ujenzi wa jengo la kuhifadhia mizigo (Cargo terminal) katika uwanja wa ndege wa Mwanza, jengo la abiria linalojengwa na  Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela na Jiji la Mwanza, jengo na mnara wa kuongozea ndege (control tower) pamoja  kipande cha  barabara  ya mita 500 cha  kurukia na kutua ndege  kilichoongozwa kukidhi  kiwnago cha kimataifa.


Vile vile walikagua karakana ya kampuni ya ujenzi wa meli na vivuko ya Songoro Marine 'Transport Boatyard'ambako kunafanyika ujenzi na ukarabati wa vivuko  mbalimbali vya Serikali vikiwamo cha MV Ilemela,  Nyerere, Butiama, Chato na vinginevyo.


Pia walitembelea miradi ya ujenzi wa barabara ya Sabasaba hadi  Buswelu yenye kilomita 9.7, barabara ya Kisesa-Usagara  ya kilomita 16.14,  ujenzi wa daraja la pande mbili za Kigongo-Busisi lenye kilomita 3.2  ambalo hivi karibuni liliwekewa jiwe la msingi na Mhe.Rais Dkt. Magufuli ambapo walimalizia  ukaguzi wa Bandari ya Mwanza Kusini  kuona ujenzi wa chelezo, meli mpya , ukarabati wa MV Victoria na MV Butiama.


Akiwa eneo la Daraja la Furahisha, Mhe.Polepole aliwaeleza wajumbe hao  kutoka Tanzania Bara na Zanzibar kwamba  baadhi ya fedha za   ujenzi wa daraja la Furahisha na upanuzi wa barabara hiyo zilitokana na uamuzi wa Mhe.Rais Dkt. Magufuki kuahirisha maadhimisho ya sherehe za Uhuru  na kuelekeza  kujengwa kwa miundombinu hiyo.


“Daraja hili na upanuzi wa barabara kutoka Ghana hadi uwanja wa ndege  vimejengwa kimkakati,  haiwezekani  mtu anatua na ndege kisha anakaa kwenye foleni, pia hapa tumejenga jengo la biashara la  kimataifa la Rocky City Mall ambapo kuna soko la madini, vile vile kuna uwanja wa mpira wa CCM Kirumba, sasa tunaposema miradi ya kimkakati  tunamaanisha kwa vitendo.


“Hii miradi inayojengwa hapa ni kwa faida ya sisi na vizazi vijazo, ipo ambayo tutaanza kuona  mafanikio kuanzia sasa lakini mingine wajukuu wetu ndiyo watafaidi na wataelezwa na watoto wetu kwamba ilijengwa na Mhe.Rais Dkt. Magufuli, kwa kasi hii ya miaka minne bila shaka CCM  itashinda kwa kishindo 2020 kwa asilimia 100, ushahidi  tumeuona kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa,”alisema.


Aidha Mhe.Polepole  aliwataka wajumbe wa NEC kuona kazi anayofanya Mhe.Rais  Magufuli  na kumsaidia kuwaeleza wananchi popote wanapopata nafasi.


Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara hiyo, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Samwel Kiboye alisema kama  isingekuwapo katiba inayoweka ukomo wa urais, Mhe.Rais Magufuli anastahili kuongoza Tanzania hadi pale anapoona inastahili mwenyewe.


“Binafsi ni muumini sana kwa wale wanaopendekeza  Rais Magufuli  aendelee kuwa  mpaka astaafu mwenyewe,  lakini kwa kuwa kuna katiba  inazuia hilo, amefanya mambo makubwa sana na nimekuwa nikiwaza hata ninapokuwa nimelala hivi ni nani ataendeleza miradi hii pale Magufuli atakapostaafu.


Baadhi ya wajumbe wakiwamo Mhe. Antony Diallo, Gasper Kikao,  Yasmin Alloo na Jamal Babu walipongeza  ujenzi wa miradi ya kimkakati ndani ya Mkoa wa Mwanza ambapo walidai  kuwa ndoto ya Mhe. Rais Magufuli  hakuna wa kuizuia kwani miradi inayojengwa imejibu kero zote za wananchi.


Waliongeza kuwa  miradi hiyo ikikamilika atakuza uchumi wa wananchi, mkoa na taifa kwa ujumla.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Songoro Marine, Major Songoro alisema kampuni hiyo imepata mageuzi ya haraka kutokana na Serikali ya awamu ya tano kuipatia zabuni nyingi kitendo kilichofanya kuongeza ufanisi katika kazi.




Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.