• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando yashauriwa kutoa elimu kuhusu Selimundu kuanzia Shuleni

Posted on: June 20th, 2022

Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Mkoani Mwanza imeshauriwa kuanza kutoa elimu kuhusiana na ugonjwa wa Selimundu kuanzia ngazi ya Shule ili Wananchi waweze kuelimika vya kutosha na kupunguza wingi wa wanaozaliwa na ugonjwa huo.


Rai hiyo imetolewa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ngusa Samike wakati wa Maadhimisho ya Siku ya Ugonjwa wa Selimundu Ulimwenguni yaliyofanyika katika Hospitali ya Bugando Mkoani humo huku akifafanua kuwa Elimu zaidi unahitajika kutokana na watu wengi kutopima kama wana vinasaba vya ugonjwa huo.


"Unakuta watu wanaamua kufunga ndoa bila kujuana vizuri nani kati yao ana vinasaba vya Selimundu matokeo yake wanakuja kujaliwa watoto wenye tatizo hilo na wakati mwingine kuibuka hali ya mshangao"


Aidha, Ndugu Samike ameikumbusha Jamii kujenga tabia ya kuwajali na kuwapenda watoto wenye tatizo hilo na siyo kuwanyanyapaa.


Aidha amewaasa jamii kuwahi kwenye Vituo vya tiba na kupata ushauri wa kitaalamu wanapogundua wamepata watoto wenye ugonjwa huo badala ya kukimbilia tiba mbadala au dawa zisizokuwa na msaada.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza DktThomas Rutachunzibwa amesema tatizo la ugonjwa huo bado kubwa kwani takwimu zinaonesha asilimia 7 ya Vifo vya watoto chini ya miaka mitano vimetokana na Selimundu.


"Tunaishukuru Serikali kwa kuwa mstari wa mbele kupambana na ugonjwa huo kwa kuboresha huduma za Maabara pamoja na Vifaa tiba" Dkt Rutachunzibwa.

Ulimwengu huadhimisha siku ya Selimundu kila mwaka Juni 19 ambapo kwa Tanzania hutumia siku hiyo kuelimishana na kuhamasisha Jamii kujenga upendo kwa Watoto wenye ugonjwa wa Selimundu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: UZINDUZI MV MPUNGU NI ISHARA YA MAENDELEO SEKTA YA USAFIRISHAJI MAJINI

    May 21, 2025
  • MSINGI WA MALEZI BORA KWA MTOTO UNAJENGA TAIFA IMARA: RC MTANDA

    May 21, 2025
  • OFISI YA MKUU WA MKOA WA MWANZA YATOA SALAMU ZA PONGEZI KWA PROF.JANABI

    May 20, 2025
  • LENGO LA HOSPITALI ZA WILAYA NI KILA MWANANCHI APATE HUDUMA MAHALI ALIPO - WAZIRI MKUU

    May 19, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.