• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Jaffo afurahishwa kasi ya ujenzi wa Jengo la Utawala Manispaa ya Ilemela

Posted on: October 22nd, 2018


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Mhe. Suleiman Jaffo amesema ameridhishwa na kasi ya ujenzi inayofanywa na uongozi wa manispaa ya Ilemela.

Mhe. Jaffo ameyasema hayo muda baada ya kutembelea jengo hilo na kulikagua akiwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella, Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Dkt. Severine Lalika, Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa hiyo John Wanga, watumishi wa Manispaa ya Ilemela na Mhandisi mshauri  wa Wakala wa majengo Benard Mayemba.

Mhe.Jaffo alimtaka Mkandarasi anayejenga jengo hilo la utawala kuhakikisha kuwa ifikapo Novemba 30 mwaka huu ahakikishe kuwa jengo hilo ambalo ujenzi wake unafanywa na Wakala wa Majengo (TBA) kupitia kikosi chake cha ujenzi cha BRIGADE kama mkandarasi mshauri uwe umekamilika.

“ Kwa kweli nimefurahishwa na kasi inayiofanywa na Mkandarasi anayejenga jengo hili, ukiliangalia limekidhi viwango niwapongeze sana," alisema Mhe.Jaffo.

Alisema Serikali imetoa kiasi cha Sh.  bilioni 38 kwa nchi nzima kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya majengo mbalimbali kwa halmashauri nchini, likiwemo jengo hilo la utawala la manispaa ya Ilemela.


Alimtaka Mkandarasi anayejenga jengo hilo la utawala, ambaye alikuwa amesimama kwa muda kwa sababu ya malipo kuendelea na ujenzi wa jengo hilo na kwamba Serikali italeta fedha za ujenzi wa jengo hilo.

Waziri Jaffo alisema jengo hilo la utawala  litakapokamilika litakuwa ni jengo kubwa na zuri la mfano lililojengwa kwa thamani halisi ya fedha kwa halmashauri zote nchini.

Kwa upande wake Mhandisi mshauri wa Wakala wa majengo Benard Mayemba alimueleza Waziri Jaffo kuwa utekelezaji wa mradi huo kwa sasa umefikia asilimia 35 na kwamba jumla ya wiki 24 zimetumika kwa ajili ya ujenzi kati ya wiki 52 za mkataba wa ujenzi huo.

Alisema hadi sasa TBA imeishapokea toka kwa Mshitiri kwa niaba ya Serikali Manispaa ya Ilemela jumla ya Sh.  996,793,934.50 malipo ambayo yamefanyika kwa awamu moja ambayo yalilipwa mwezi April mwaka huu ambapo utekelezaji wa mradi ulianza rasmi Mei 6 mwaka huu na kwamba kiasi cha Sh.bilioni 3.8 kinatarajiwa kutumika kwenye ujenzi wa jengo hilo la utawala.

Aidha Muyemba alisema kuwa licha ya juhudi zinachukuliwa na manispaa na wakala katika utekelezaji wa mradi huo, bado mradi huo unakabiliwa na changamoto kuu tatu ambazo ni ukosefu wa fedha kutokana na kutegemea ruzuku ya Serikali, upatikanaji duni wa maji kutoka Mamlaka za maji na uhaba wa vifaa vya ujenzi.

“ Kutokana na changamoto ya upatikanaji wa maji, Wakala kwa sasa unanunua maji kwenye ma-bouza na tayari Mshitiri ameishataarifiwa juu ya tatizo hili, ingawa maeneo haya ulipo mradi huu yanakumbwa na tatizo la jumla la uhaba wa maji,” alisema.

Kazi zinazotekelezwa kwenye mradi huo ni kujenga uzio kuzunguka eneo la mradi, kufanya setting ya jengo, kuchimba eneo la kujengea, matayarisho ya kujenga vitako vya nguzo ukuta wa msingi wa jengo na kumwaga zege la jamvi la chini kwa asilimia 100.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.