• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Jamii ina mchango mkubwa wa kuutokomeza ugonjwa Ukimwi: RC Makalla

Posted on: December 1st, 2023

Jamii ina mchango mkubwa wa kuutokomeza ugonjwa Ukimwi: RC Makalla


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.CPA. Amos Makalla amesema kazi ya kuutokomeza ugonjwa wa Ukimwi siyo ya Serikali pekee bali jamii bado ina mchango mkubwa wa kupambana nao na kuelimishana kwa njia mbalimbali.

Akizungumza kwa niaba yake leo Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Seni Ngaga wakati wa Maadhimisho ya siku ya Ukimwi Duniani yaliyofanyika ki-mkoa wilayani humo amesema bado mkazo wa elimu unahitajika kutokana na maambukizi hayo kuchangiwa na sababu mbalimbali ikiwemo kuendekezwa kwa mila na desturi zilizopitwa na wakati na ngono zembe.

"Mkoa wetu bado unashika nafasi ya juu ya maambukizi ambayo ni asilimia 7.2 hii maana yake bado tuna jukumu kubwa la kuhakikisha kasi hiyo inashuka au inakwisha kabisa," Mhe.Ngaga

Ameongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na Asasi zisizo za Kiserikali zinazopambana na ugonjwa huo na magonjwa mengineyo yasiyoambukiza itaendelea kushirikiana nazo ili kulinda nguvu kazi ya Taifa.

"Wizara ya afya imetoa pia kipaumbele kwa ugonjwa wa homa ya ini ambao umekuwa tishio pamoja na yale yasiyoambukiza, msisitizo wetu ni kuhakikisha jamii inaendelea kujengewa uwezo wa uelewa," Dkt.Florence Nduturu, mwakilishi kutoka Wizara ya afya.

Amewataka wale wote watakaobainika na ugonjwa huo kuanza kutumia dawa kwa usahihi na siyo kutokomea mara baada ya vipimo kuonesha wana maradhi hayo na badala yake kwenda kutumia tiba zisizo sahihi.

Akitoa ushuhuda wakati wa Maadhimisho hayo Deus Sahani anayetokea Baraza la watu wanaoishi na ugonjwa wa Ukimwi, amebainisha hadi sasa ana miaka 16 akiwa na maradhi hayo na amekuwa na afya njema kutokana na kuzingatia unywaji wa dawa kwa usahihi huku akiendelea na shughuli zake za kuipatia familia yake kipato bila tatizo.

"Bado kuna changamoto ya watu mara baada ya kupima na kugundulika wanakwenda kupata matibabu kwa siri na anapokuja kuzidiwa anarudi Hospitali huku akiwa amedhoofika sana na mwishowe kukutwa na mauti", amefafanua ndugu Sahani wakati akihimiza jamii kupambana na ugonjwa huo.

Kila Disemba Mosi Tanzania inaungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya Ukimwi huku mwaka huu kauli mbiu ikisema "Jamii  iongoze katika kuutokomeza Ukimwi".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.