• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

JENGENI MALENGO MAKUBWA KATIKA UFUGAJI WA SAMAKI KWA VIZIMBA:RAS MWANZA

Posted on: September 18th, 2024

JENGENI MALENGO MAKUBWA KATIKA UFUGAJI WA SAMAKI KWA VIZIMBA:RAS MWANZA


Katibu Tawala wa mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amevishauri vikundi vya vijana vinavyojihusisha na ufugaji wa samaki kwa njia ya Vizimba kujenga tabia ya kuwa na mpango biashara ambao utawasaidia kupiga hatua kubwa kiuchumi.

Akiwa katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo leo Septemba 18,2024 wilayani Nyamagana,mtendaji huyo wa Mkoa amebainisha bila ya kujiwekea dira katika ufugaji huo itawachukua muda mrefu kupiga hatua.

"Nawapongeza kikundi cha Vijana Agro Group nimesikia taarifa yenu na jinsi mnavyo nufaika kwa kipato,na nidhamu ya marejesho ya mkopo wa asilimia 10, sasa muanze kuwa na mkakati wa kikundi kupiga hatua kibiashara,"amesisitiza Balandya wakati akizungumza na vijana wanufaika na mradi wa vizimba eneo la Luchelele

Aidha amemshauri Mkurugenzi wa Jiji la Mwanza kuona namna ya kuwawezesha vikundi vya vijana mtaji mkubwa zaidi kupitia mpango biashara wao kulingana na mapato yao ya ndani ya halmashauri hiyo hali itakayowasaidia katika kupiga hatua zaidi kiuchumi.

Amesema mchakato wa kujengwa kiwanda cha kuchakata chakula cha samaki kipo mbioni kujengwa mkoani Mwanza hali ambayo itapunguza mzigo wa gharama kwa wanufaika

"Tumefanikiwa kupata sh milioni 86 katika mavuno ya samaki mwaka jana na juzi na tumefanikiwa kurejesha shs milioni 22 hadi sasa katika mkopo wa shs milioni 150 tuliopatiwa,"Daisy Ulaya, mnufaika na Katibu wa kikundi cha Vijana Agro Group.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe.Amina Makilagi amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya ufugaji wa samaki kwa njia ya kisasa na kutanua wigo wa ajira kwa vijana.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.