• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Jiji la Mwanza wapongezwa kwa ujenzi wa Madarasa ya ghorofa

Posted on: January 17th, 2023


Halmashauri ya Jiji la Mwanza wilayani Nyamagana wamemkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima vyumba vya madarasa 196 yaliyojengwa kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 kwa thamani ya Shilingi Bilioni 3.92.

Akizungumza kwenye hafla ya mapokezi ya vyumba hivyo iliyofanyika kwenye shule ya Sekondari Igelegele Mkuu wa Mkoa ametumia wasaa huo kumshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuwajali wananchi wa Mwanza na watanzania kwa ujumla kupitia Miradi ya Ujenzi wa Miundombinu kwenye sekta ya Elimu.

Mhe. Malima amewapongeza viongozi wa Halmashauri na Wilaya kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa vyumba vya madarasa na maamuzi ya kujenga Madarasa katika mfumo wa ghorofa kwani inasaidia kutumia ardhi vizuri  Wananchi wanaongezeka hivyo matumizi ya ardhi yanazidi kukua.

Amewasihi wazazi, walezi, walimu na wadau wote wa sekta hiyo kuhakikisha watoto wanapata elimu bora waliyoandaliwa kwa kuwajengea Miundombinu hivyo wanafunzi wanapaswa kuongeza kiwango cha ufaulu na ametoa wito kwa wanafunzi hasa wa kike kujibidiisha kwenye elimu na wazingatie kusoma masomo ya Sayansi.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Makilagi amemshukuru Mhe. Rais kwa kuwaondolea upungufu wa vyumba vya madarasa uliyokuwepo siku za nyuma kwa kuwaletea fedha za Ujenzi wa Madarasa 196 kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na ametoa wito kwa wazazi kuwapeleka watoto shule.

"Ni ukweli usiopingika, Mhe. Rais anatupenda sana maana ni mwaka jana tu ametuletea zaidi ya Bilioni 2 kujenga Madarasa hatujakaa sawa ametuletea tena zaidi ya Bilioni 3 na kufanya tupunguze msongamano wa wanafunzi darasani kwani tumeondoa upungufu tuliokua nao wa Madarasa 400 na sasa tatizo hilo halipo." Mhe. Makilagi.

Mapema asubuhi, Mhe. Mkuu wa Mkoa amekagua Ujenzi wa Vyumba vya Madarasa 6 yanayojengwa kwa Mfumo wa ghorofa kwenye shule ya Sekondari Mkuyuni  kata ya Mahina na amewapongeza walimu na Viongozi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri wa Madarasa ya kisasa.

"Kwa niaba ya wanafunzi wenzangu tunamshukuru Mhe . Rais kwa kutuletea fedha za ujenzi wa vyumba vya Madarasa na Uongozi wa Mkoa, Wilaya na Halmashauri kwa usimamizi mzuri na nawasihi wanafunzi wenzangu tuyatunze Madarasa haya yaweze kutusaidia." Semfroza Baraka, Mwanafunzi wa kidato cha nne Igelegele.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.