• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kamati ya Uwekezaji Yaridhishwa utekelezaji mradi wa Daraja la JPM*

Posted on: March 25th, 2023



Kamati ya Kudumu ya Bunge ya  Uwekezaji wa Mitaji ya Umma imefanya ziara kwenye mradi wa ujenzi wa Daraja la JPM( Kigongo- Busisi) Mkoani Mwanza na kuridhishwa na maendeleo ya utekelezwaji wa mradi huo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe.Jerry Silaa ameyasema hayo leo Machi 25,2023  baada ya kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo unaogharamiwa na Serikali kwa asilimia 100 kwa gharama ya Sh bilioni 716.33 na kufikia asilimia 70 ya utekelezwaji.

Mhe. Silaa amesema mradi huo unajengwa kwa fedha za serikali ili kuwanufaisha wananchi hivyo wahusika wote wanaousimamia ikiwemo Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi pamoja na Wakala wa Barabara Tanzania(Tanroads) wahakikishe unakamilika kwa wakati, wananchi waweze kuutumia na kupunguza muda wa kuvuka  Ziwa Viktoria kwa dakika nne badala ya saa mbili wanazozitumia sasa.

"Nasisitiza tena daraja hili linajengwa kwa fedha za serikali tunaomba likamilike Februari  2024 kama ilivyo kwenye mkataba ili wananchi wanufaike nalo lakini pia tunaipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi hakika inafanya kazi kubwa tumekagua mradi huu na mingine ambayo inatekelezwa kwenye mikoa mingine tumepata moyo kwamba nchi hii inajengwa na inafunguka kiuwekezaji,”amesema Mhe. Silaa.

Aidha Mhe. Silaa ameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha miradi yote inaendelea kutekelezwa.

“ Hakuna mradi uliosimama na maendeleo yote yanayofanyika yanafanyika katika kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM),"amesema Mhe. Silaa.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi Balozi  Mhandisi Aisha Amour  amesema hawataongeza muda kwa mkandarasi anayetekeleza mradi huo hivyo ahakikishe unakamilika kwa wakati na ukiwa na ubora kama ilivyo kwenye mkataba.

“Namwagiza mkandarasi ahakikishe mraadi huu unakamilika kwa wakati maana haujawahi kukwama kwa kukosa fedha hivyo tunatarajia ifikapo Februari 24, 2024 atakuwa ameukamilisha ili wananchi ambao wameusubiri kwa muda mrefu waanze kuutumia.


“Pia tunawashukuru sana wabunge kupitia kamati hii ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma  kufika hapa kwenye mradi kuutembelea na kuukagua maana mnawawakilisha wananchi hivyo wakisikia kutoka kwenu watajua kwamba kazi inaendelea tunawaahidi kwamba utakamilikakwa wakati maana tumekwishamsisitiza mkandarasi azingatie muda" amesema Mhadisi Amour.

Awali akitoa taarifa fupi ya Mkoa wa Mwanza kwa  wajumbe wa Kamati hiyo kwa niaba ya  Mkuu wa Mkoa  huo, Mhe. Paul Chacha ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, alisema ujenzi wa mradi wa daraja la JPM ukikamilika utasaidia kuchochea maendeleo ya ukanda wa ziwa pamoja na taifa kwa ujumla, utaunganisha barabara kuu ya Usagara-Sengerema katika Ziwa Viktoria na mikoa ya Magharibi pamoja na nchi jirani za Rwanda, Burundi na Uganda.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.