• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kamati za Maadili za maafisa wa Mahakama zatoa mafunzo Mwanza

Posted on: February 4th, 2020


Wakuu wa Wilaya na Makatibu Tawala wameshauriwa kuwa  karibu na shughuli za mahakama ili  kuhakikisha ikitenda  haki pasipo kumuonea mwananchi huku wakitakiwa kutengeneza mfumo wa masikilizano na kutoingilia mfumo wa kisheria ili kuleta utulivu na ushamilishaji utendaji haki.

Akizungumza katika kikao kazi cha pamoja kilichowakutanisha Wakuu wa Wilaya ,Makatibu Tawala wa Wilaya pamoja na Watendaji wa Mahakama, kujadili muundo na utendaji kazi wa kamati za maadili za mahakimu wa mikoa na wilaya, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella alisema ofisi ya Mkuu wa wilaya haikatazwi kutengeneza mifumo ya mawasiliano na siyo kuingilia mifumo ya kisheria lakini mifumo ambayo italeta utulivu itashamilisha utoaji wa haki bila kuathiri nafasi ya kila muimili.

Aliongeza kuwa mahakama nayo itahitaji mifumo mingine kwenye utekelezaji wa maelekezo yake hivyo cha msingi ni kuaminiana ili watu wote watambue na kuamini kile kinachofanywa na mahakama kuwa ni haki.

kwa upande wake Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza Mhe. Joachim Tiganga ameagiza mahakimu kufanya kazi kwa uzalendo na uadilifu bila kwenda kinyume na taratibu za kisheria  na maadili ya kazi ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu kwa uharaka na  usawa.

Alisema kila hakimu ni kiongozi kwa mujibu wa sheria hivyo jukumu lake ni kuhakikisha watu wote wanaofanya kazi chini yake na kutekeleza maadili kama ambavyo sheria inavyowataka.

“Ikitokea mtumishi yoyote anayefanya kinyume na maadili na asichukue hatua anachukuliwa na yeye kuwa amekubaliana na uovu uliofanyika na yeye anaweza kuchukuliwa hatua kama kosa la kimaadili”alisema Mhe. Tiganga.

 “Maamuzi ya hakimu yamejengwa juu ya imani pindi ambapo imani yake imeondoka kwake anajukumu la kujiondoa kwenye kesi au shauli lililopo mbele yake”aliongeza.

Akizumgumza kwa niaba ya wenzake Mkuu wa wilaya ya Magu Mhe. Dkt.Philemon Sengati alisema watahakikisha wanayafanyia kazi maagizo yote waliopatiwa kwa weledi zaidi na kuhakikisha watumishi wa mahakama wanafanya kazi kwa kuzingatia sheria taratibu na maadili ya utumishi wa umma .

“Sisi kama viongozi na wenyevita wa hizo kamati tuta hakikisha baada ya hii semina tunakwenda kuwahamasisha watumishi wetu kufanya kazi kwa nidhamu na weredi mkubwa katika kuwatendea haki wananchi”alisema Dkt.Sengati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.