• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kamilisheni Miradi ya maji - Aweso

Posted on: May 6th, 2021

Waziri  wa Maji Mhe.Jumaa Aweso amemtaka Mhandisi Mshauri wa mradi wa tenki la maji la unaogharimu billion 6 Buswelu  Andrew Mwakagenda kujitafakari  baada ya kuongopa wanafanya kazi hadi siku ya jumapili.

Kauli hiyo ameitoa alipotembelea mradi huo na kusema hakuna Kazi inayofanyika jumapili bali kawaleta wafanyakazi ili kuonyesha wanafanya kazi wakati hakuna wanachofanya .

" Hapa hakuna Kazi mnayoifanya kelele ni nyingi sana Mwanza serikali inaleta fedha nyingi ilu kukamilisha miradi itakayo wanufaisha wananchi kazi ifanyike kama hauwezi utatupisha tunapokuja kukagua mradi msituuzie mbuzi kwenye gunia kwa kutuonyesha mnafanya kazi kumbe amna mnachofanya tukiondoka na nyie mnaondoka " alieleza Aweso.

Pia aliiagiza MWAUWASA na RUWASA Mwanza washirikiabe kuhakikisha wanakamilisha mradi wa Igongwe na Kahama kwa wakati ili wananchi wapate maji ,pia kwa washauri wote wa miradi aliwataka kuacha maigizo bali wafanye kazi kwa bidii na kukamilisha miradi yote kwa wakati na watakaposhindwa kujipanga watasaidiwa.

Alisema adhima ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuona wananchi wanapata maji safi na salama hiyo ndio Kiu yake hivyo wakandarasi wote watambue hakuna muda wa nyongeza waache janjajanja bali wachape kazi.

Naye Kaimu Mkurugenzi  Mtendaji wa MWAUWASA  Mhandisi Leonard Msenyele alisema  katika mradi wa Buswelu ambao utagharimu Billion 6 unatarajiwa kukamilika mwezi  October mwaka huu huku kazi zilizopangwa kufanyika zikiwa ni kulanza bomba la Plastic na chuma kutoka kituo cha kusukuma maji kiseke hadi tanki la Buswelu kilimita 9.51 ambapo wananchi zaidi ya  100,000 watanufaika .

Alisema uzalishaji wa Maji Jijini hapa kupitia mtambo wa kapripoint wanazalisha wastani wa lita million 90 kwa siku huku mahitaji halisi yakiwa ni lita million 150 kwa siku hivyo bado wanakabiliwa na upungufu wa takriban lita million 60 kwa siku

" Ili kuweza kutatua ilo tatizo la upungufu wa lita million 60 serikali inatekeleza ujenzi wa chanzo kingine kipya kilichopo eneo la Butimba Magereza." Alieleza Msenyele.

Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba alisema Wizara itafatilia utekelezaji kwa ukaribu kwani lengo lao kubwa ni miradi ikamilike kwa wakati.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella alisema Mwanza inakabiliwa na changamoto ya maji hiyo inatokana na maendeleo kwenda kwa kasi kubwa.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.