• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

KERO YA MAJI MWANZA SASA KUTOWEKA KABISA: RC MAKALLA

Posted on: January 8th, 2024

KERO YA MAJI MWANZA SASA KUTOWEKA KABISA: RC MAKALLA


*Ampongeza Rais Samia kwa kutoa fedha nyingi za Miradi ya maji*


*Asema mikakati ipo Mwanza kuwa ya kwanza  kuchangia pato la Taifa*


*Miradi yote ya kimkakati ipo mbioni kukamilika na kuzidi kuipaisha Mwanza kiuchumi*


*Ndege ya kubeba Minofu ya Samaki kuanza kutoa huduma hivi karibuni*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla leo Januari 8, 2024 ameipokea Kamati ya kudumu ya Bunge ya bajeti na katika mazungumzo yake amesema kero ya muda mrefu ndani ya Mkoa wa Mwanza sasa kutoweka baada ya kukamilika mradi mkubwa wa chanzo cha maji cha Butimba.


Akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Daniel Sillo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Makalla amebainisha mradi huo wa Butimba wenye mitambo ya kisasa ambao upo asilimia 100 kukamilika utatoa kwa siku lita milioni 148 kwa siku.

"Mhe. Mwenyekiti wa kamati Mkoa wa Mwanza mradi huu sasa utawanufaisha wakazi wa Nyamagana, Ilemela, Misungwi na Magu, tunaipongeza sana kamati yako kwa usimamizi mzuri wa fedha hizi za bajeti zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya maendeleo ya wananchi," CPA. Makalla


Akizungumzia kwa ufupi miradi ya kimkakati inayoendelea kutekelezwa Mkoani humo, Mkuu huyo wa Mkoa amesema ukarabati wa uwanja wa ndege utaanza Februari mwaka huu na kukamilika Juni na mizigo ya minofu ya samaki itaanza kusafirishwa kutoka uwanja huo kuanzia  Machi mwaka huu badala ya kuanzia uwanja wa Entebe na Nairobi.

"Tayari tumefanya mazungumzo na uongozi wa ATCL kuhusiana na usafirishaji wa mizigo hiyo baada ya kupata usumbufu wa kwenda kuisafirisha mbali na uwanja huu wetu wa Mwanza," amesisitiza Mkuu huyo wa Mkoa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge Mhe. Daniel Sillo amesema kamati yake imefika Mwanza ikiwa ni sehemu ya majukumu yake ya kukagua miradi yote inayotekelezwa kwa fedha za Serikali ili iweze kujionea maendeleo  na changamoto zake na baadaye kutoka ushauri kwa Serikali.

"Tuna kazi ya kuhakikisha mipango yote ya maendeleo ya kiuchumi hapa nchini inatekelezeka kama ilivyokusudiwa tupo Mwanza kukagua mradi wa chanzo cha maji Butimba, Rais wetu amekuwa mstari wa mbele kutafuta fedha na kuzitoa kwa maendeleo ya wananchi hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tuna muunga mkono kwa kusimamia ipasavyo,"Mhe. Sillo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.