• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kivuko Cha MV.Ukara Hapa Kazi Tu chaingizwa ziwani kwa majaribio

Posted on: October 13th, 2020

Neema yawashukia wakazi wa visiwa vya Ukara na Ukerewe mkoani Mwanza baada ya serikali  kutatua tatizo la usafiri lililokuwa likiwakabili baada ya Mv.Nyerere kuzama, imetengeneza kivuko kipya  chenye uwezo wa kubeba abiria 300 ,magari 10 na mizigo tani 100 kilichogharimu billion 4.2.

Kivuko hicho cha Mv.Ukara hapa kazi tu kimetengenezwa  na kampuni ya Songoro Marine iliyopo Jijini hapa kimeingizwa ziwani kwa ajili ya kufanyiwa majaribio ili kuanza rasmi safari zake kati ya kisiwa cha UKara kwenda Ukerewe.

Akizungumzia na waandishi wa habari wakati wa kuingiza kivuko hicho majini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(Sekta ya Ujenzi), Elius Mwakalinga alisema,kivuko hicho kitaanza kazi baada ya siku tatu kwa sasa kinafanyiwa matazamio ya kuona Kama kinaweza kufanya kazi.

" Kivuko hiki kinabeba wananchi ambao serikali inawathamini sana kuanzia maisha yao pamoja na mali zao hivyo tusingependa masuala mengine kama yaliyotokea yatokee tunamuomba Mungu atuepushe lakini ninachokiona kinaingia majini ni kivuko ambacho tumelipia billion Sh.4.2kama.kingenunuliwa nje ya nchi kingegharimu Sh. Bilioni 22 lakini kampuni ya ndani ya Songoro Marine ilikubali kukitengeneza kwa gharama ya hizo" anasema Mwakalinga.

Aliongeza kuwa kivuko hicho kitafanya idadi ya vivuko kufikia 16 katika ziwa Viktoria na kwamba hiyo ni ahadi ya Rais John Magufuli ,na kuongeza kuwa jumla  ya Sh. Bilioni 10 zimetumika kwa  ajili ya kujenga   vivuko mkoani  Mwanza Ili kuhakikisha wananchi wanaoishi katika visiwa 38  wanakuwa na usafiri wa uhakika,akitaja vivuko vingine vilivyonunuliwa miaka ya hivi Karibuni kuwa ni pamoja na Mv. Ilemela,Mv. Chato na Mv. Ukara.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) Japhet Masele alisema, kwa sasa wana vivuko 30 ambavyo vinafanya kazi katika Maeneo mbalimbali ya  nchi, baada ya kivuko hicho cha MV Ukara kuingizwa ziwani kitaendelea kufanyiwa mazoezi na kuhakikiwa  na watalaam kwani kukamilika kwa kivuko hicho ni ukombozi kwa wakazi wa Ukara.

Akizungumza baada kuwekwa kivuko hicho majini, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella alisema, ni takriban miaka miwili kivuko hicho kimekamilika hivyo nchi yetu imshukuru Mungu sana kwa kupata kiongozi mahili mwenye maamuzi,maono na anayeguswa na shida za wananchi.

 Anasema wananchi wa Ukara sasa wamepata usafiri ambao utakabidhiwa kwao hivi Karibuni pia alipongeza juhudi za Mhe.Rais John Magufuli kwa namna ambavyo anawasaidia wananchi wa visiwa vya Ukerewe na maeneo mengine ya nchi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Cornel Magembe alisema tangu ilipotokea ajali ya Mv.Nyerere mwaka 2018 wananchi walikabiliwa na shida ya usafiri Kati ya Ukerewe na Ukara


Alisema kwa niaba ya wananchi wa Wilaya yake wanatoa  shukurani kwa Rais  baada ya kutekeleza ahadi yake aliyoitoa baada ya kuielekeza Wizara ya Ujenzi kuunda kivuko kipya  ambacho itatatua changamoto ya usafiri katika eneo hilo  .

" Wananchi walikuwa wanaisubili kwa hamu kweli hakika leo Kisiwa chote cha Ukerewe kitakuwa na furaha ambayo haiwezi kuelezeka nimeambiwa tarehe 19 kivuko hiki kitafika Ukerewe hivyo nawaomba wananchi wote wa visiwa vyote wajitokeza kwa wingi kuipokea hakika ni Jambo lenye Neema,tunaishukuru awamu ya tano imetekeleza ahadi zake kwa vitendo" anaeleza Magembe.

Major Songoro ni Mkurugenzi wa Songoro Marine anasema wanaishukuru serikali kwa kuwapatia kazi ,kivuko kipo tayari kwa Sasa kipo kwenye majaribio ya mwisho ili kuhakikisha usalama wake ili kiweze kuanza kutoa huduma kwa wananchi .

" Serikali inapowekeza kwenye vitu hivi vinaenda kujenga uchumi mkubwa sana pia sisi tunafuraha kubwa kuwa miongoni wa kujenga uchumi wa watu wa Ukara na Ukerewe" anaeleza Songoro.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.