• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kivulini Yakabidhi Kompyuta 10 serikalini

Posted on: August 27th, 2019

Shirika   la Kutetea Haki za Wanawake na Watoto (Kivulini) limetoa  msaada wa kompyuta mpakato 10 katika  vitengo maalum  vinashughulikia  masuala ya ukatili wa jinsia kwenye  ofisi  ya mkuu wa mkoa wa Mwanza,  Kamanda wa Polisi mkoa huo,Hospitali ya Rufaa ya mkoa –Sekoutoure na  Wilaya ya Misungwi.

Makabidhiano hayo yalifanyika  kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Kivulini, Yassin Ally na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Christopher Kadio ambaye  pia aliwakabidhi wakuu wa vitendo husika  na kuwataka kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa ili  kutekeleza Mpango Kazi wa Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto  2017-2022 (MTAKUWWA).

 Akizungumza baada ya makanidhiano hayo, Ally alisema lengo la kutoa msaada wa vifaa hivyo ni kutaka kuimarisha  mfumo wa data-kazi ili kuhifadhi kumbukumbu za vitendo vya ukatili  vinavyotokea ndani ya jamii na kufikia lengo la taifa la kupunguza ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Ally alisema  amelazimika kutoa  msaada huo katika idara hizo kwa sababu  katika kufanya  kazi ya mapambano ya kutokomeza vitendo vya ukatili, alibaini kuwapo na changamoto ya watendaji wa Serikali kukosa sehemu salama ya kuweka kumbukumbu zao ambapo   nyingi huandikwa kwenye makaratasi na mara nyingine zinapotea.

“ Vitendo hivi vya ukatili bado ni tatizo kubwa sana, ili kuona ukubwa wake nendeni polisi mkaone mashauri yanayopokelewa lakini mengi yanaishia huko huko katika hatua ya upelelezi  na machache ndio yanafikishwa mahakamani lakini yanayopata mafanikio yanaweza kuwa 20 kati ya 100.

“Ndiyo maana  kama shirika la Kivulini tumeona katika kutimiza malengo yetu tumekuwa tukishirikiana na  polisi, hospitali na Ofisi ya Mkuu wa mkoa , wilaya na idara zake, hivyo tumenunua kompyuta 10 zenye thamani ya Sh milioni 12, namkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa ambaye  atazikabidhi kwa wahusika, haiwezekani tukawa tunapamba na jambo huku hakuna sehemu ya kuweka kumbukumbu.

 Ameongeza kuwa watumishi wa Serikali hasa sekta ya afya bado hawapo tayari kujitokeza kutoa ushahidi mahakamani pale wanapohitajika jambo ambalo linaathiri malengo ya kutokomeza vitendo hivyo, vile vile aliwaomba polisi kuongeza jitihada za upelelezi kwani mashauri mengi yanaishia mikononi mwao.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa huo, Christopher  Kadio amesema msaada uliotolewa na Kivulini ni mkubwa ambapo aliwataka wajumbe wa kamati ya ulinzi ya wanawake na watoto ngazi ya mkoa kutekeleza majukumu yao ipasavyo na kuhakikisha wanakomesha vitendo vya ukatili wa ngono, kihisia, kimwili na kiuchumi.

“Hakikisheni sasa mnatanua wigo wa kupambana na vitendo hivi maana  mtoto akishafanyiwa ukatili tayari inaathiri ukuaji na malengo yake, sote tunajua  mpango wa serikali umejikita katika maeneo nane ya kufanyia kazi ikiwamo  kuimarisha uchumi wa kaya, kukomesha mila na desturi mbaya, kuimarisha malezi, kujichukulia sheria, utoaji wa huduma kwa waathirika, kuratibu na kutathimini zoezi hilo.

“Kwa kuwa vitendea kazi vimepatikana, utaratibu  ni kwamba vikao vya mrejesho vitakuwa vikifanyika kwa kila robo ya mwaka ili kuona mafanikio yake kufikia 2022, naomba kila mjumbe wa kamati ya ulinzi wa wanawake na watoto ya mkoa, aone ana wajibu wa kuleta mbinu ya kumaliza tatizo hili,”alisema.

Naye Mwakilishi wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Murilo,  Slyvester  Ibrahimu, alisema licha ya kuwapo na mapambano ya vitendo vya ukatili lakini takwimu za makosa yaliyoripotiwa polisi yanaonekana kupanda  tangu 2016 hadi Juni 2019.

Alisema mwaka 2016 makosa ya unyanyasaji na ukatili kwa watoto yalikuwa ni 1165, 2017 yalikuwa 1287, 2018 ilikuwa1683 na  mwaka huu kufikia Juni yameripotiwa 1012.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.