• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maafisa Mazingira Kanda ya Ziwa wapewa somo Mwanza

Posted on: May 18th, 2023

RAS Balandya awataka Maafisa Mazingira kuwa wabunifu wa utunzaji na kuyalinda Mazingira


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Ndg.Balandya Elikana amewataka Maafisa Mazingira wa Mikoa na Halmashauri Kanda ya Ziwa kutumia vizuri elimu wanayopata kuhusu Mazingira kuja na mikakati kabambe ya utunzaji na kuyalinda kwa faida ya vizazi vijavyo.

Akizungumza leo  kwa niaba yake kwenye ufunguzi wa Warsha ya Kikanda ya kukuza uelewa kuhusu mpango wa Hifadhi na usimamizi wa Mazingira mwaka 2022-2023,Katibu Tawala Msaidizi,Mpango na Uratibu,Ndg.Joachim Otaru amesema kumekuwepo na kasi ya uharibifu wa Mazingira kwenye maeneo mbalimbali hapa nchini,hivyo ni wajibu kwa Maafisa Mazingira kuonesha matokeo chanya kupitia elimu wanayopata kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

Otaru amebainisha Mkoa kama wa Mwanza bado utupaji wa taka ngumu kwenye Ziwa Victoria imezidi kuongezeka na shughuli za Kilimo kando kando ya vyanzo vya maji ndani ya mita 60 ya maziwa na mito,yote hayo yanahitaji kufanyiwa kazi kupitia njia mbalimbali ili wananchi waelimike vizuri.

"Niipongeze Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kuwaleta Wataalamu wake hapa Mwanza na kutoa elimu hii,Ziwa letu Victoria kuna mambo mengi ya hovyo yanayofanyika ukiwemo Uvuvi haramu,niwaombe Maafisa Mazingira punguzeni muda mwingi wa kukaa Ofisini badala yake fanyeni kazi kwenye maeneo hayo yaliyopo kwenye tishio la uharibifu",Otaru

"Njia mojawapo ya kuwa na Mazingira bora na salama ni kama hii ya utoaji wa  elimu,tusirudi nyuma kuwaelimisha wananchi wetu,changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi yanachangiwa na sisi wenyewe kama ukataji wa hovyo wa miti",Martha Kalowela,Afisa Mazingira kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais.

Naye Afisa Mazingira kutoka Geita,Tito Mlela amesema elimu kama hiyo inazidi kuwaongezea  uwezo na wao kupata nafasi ya kuwasilisha baadhi ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwemo utungwaji wa Sheria ndogo ndogo ili ziwasaidie kutekeleza majukumu yao.

"Mkoa ninao toka una shughuli nyingi za uchimbaji wa Madini,sehemu hizo uharibifu wa Mazingira ni wa kiwango cha juu,naamini baada ya Warsha hii nitapata la kujifunza ambalo kitakuwa na tija eneo langu la kazi.

Warsha hiyo imewashirikisha Maafisa Mazingira wa Mikoa na Halmashauri kutoka Mikoa ya Mwanza,Geita,Simiyu,Mara na Kagera.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.