• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA YAPUNGUA : RC MTANDA

Posted on: May 29th, 2024

MAAMBUKIZI YA UKIMWI MWANZA YAPUNGUA : RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewashukuru wahisani kwa kusaidia juhudi za kupunguza maambukizi kwa vifaa na rasilimali watu kwa zaidi ya Bilioni 10 kwa kujenga Maabara ya Kisasa ya Uchunguzi wa Magonjwa hususani virusi vya Ukimwi

Ametoa pongezi na shukrani hizo tarehe 29 Mei, 2024 kwenye hafla ya kukabidhi Maabara ya Upimaji Usugu wa dawa za kufubaza virusi vya Ukimwi katika hafla iliyofanyika kwenye viwanja vya Hospitali ya Kanda Bugando.

Ameongeza kuwa misaada mbalimbali imesaidia juhudi za serikali za kupunguza maambukizi nchini hadi kuifanya Mwanza kushuka Maambukizi kutoka asilimia 7.2 mwaka 2017/18 hadi 4.7 kwa sasa hivyo uongozi wa Mkoa unathamini sana.

Ameongeza kuwa, Maabara hiyo itasaidia kupima vimelea na maambukizi na kutoa dira kwa afua mbalimbali za kuzuia maambukizi ya Ugonjwa wa UKIMWI na kwamba mikoa ya kanda ya ziwa wamepata sehemu mahususi kwa tiba na uchunguzi.

Mganga Mkuu wa Mkoa Thomas Rutachunzibwa amesema amebainisha furaha ya sekta ya Afya kwa kushirikiana na wahisani hao kwa dahari ya miaka hususani kwenye utaalamu na minundombinu ya kufubaza maambukizi ya Ukimwi.

Mkurugenzi wa ICAP nchini, Haruka Maruyama ameshukuru uongozi wa Mkoa na Bugando kwa kukubari uwepo wa miundombinu hiyo muhimu kwa ajili ya kupima magonjwa mbalimbali kwa Watanzania kwani itasaidia kuboresha huduma hizo kwenye ukanda wa ziwa.

Akimuwakilisha Balozi wa Marekani nchini, Mtendaji wa CDC nchini Dkt. Mahesh Swaminathan amesema wanayo furaha kuwepo nchini kwa miaka 15 na kwamba wamesaidia takribani Shilingi Bilioni 4 kutekeleza mradi huo Bundando Hospitali.

Mkurugenzi wa Buganda Dkt.  Fabian Masaga amewashukuru wahisani PEPFAR na CDC kwa kushirikiana na ICAP Global Health kuwaboreshea maabara ya kisasa na rasilimali watu na kusaidia kupunguza matumizi ya nishati ya Umeme na Maji.

Ameongeza kuwa Bugando ina maono ya kukomesha magonja ya kuambukizwa pamoja na yake ya ukanda hivyo msaada wa maabara utasaidia juhudi hizo kwani pamoja na miundombinu wamewajengea uwezo watumishi wa maabara hiyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.