• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maandalizi GLITE Yazinduliwa Mwanza

Posted on: March 4th, 2020

Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Hamissi Kigwangala amezindua rasmi maandalizi ya maonesho ya kimataifa y a utalii katika Ukanda wa Maziwa Makuu na jukwaa la uwekezaji katika sekta hiyo,yanayotarajiwa kufanyika juni 19 hadi 21 mwaka huu,katika uwanja wa CCM Kirumba Mkoani Mwanza, ambapo aliwahamasisha wawekezaji wa ndani kutumia jukwaa hilo kama fursa ya kuvitambua na kuvitangaza vivutio vilivyopo nchini.

Akizungumza  wakati akizindua nembo maalum ya maonesho hayo ya kimataifa yaliyofanyika  jijini Mwanza yanayotambulika kwa jina la Great Lakes International Tourism Expo(GLITE) yanayolenga kuvitanganza vivutio vya utalii vya maeneo ya maziwa makuu yatakayokuwa yanafanyika kila mwaka ambayo yatahusisha mikoa ya Mwanza,Geita,Simiyu,Shinyanga,Kagera,Mara,Tabora na Kigoma Dkt.Kigwangala ,alisema ili kuhakikisha fursa ya utaliii inaenea kwa nchi nzima,kupitia maonesho hayo yatatangaza vivutio hivyo na kuwavutia wawekezaji ambapo wanatarajia kuweka mabanda zaidi ya 150 .

Alisema,zaidi ni kutangaza vivutio vilivyopo pamoja na kutangaza fursa mbalimbali ambazo zinapatikana katika mikoa hiyo hatimaye kuwataembeza wageni ambao watakuja kwenye maonesho ili washuhudie kwa macho kile kilichotangazwa na kuwaeleza taratibu za uwekezaji ambao watajitokeza ili waelewe kwenye ukanda huu kuna fursa zipi na taratibu zipoje za kupata maeneo ya kuwekeza.

“Mazao ya utalii ni vitu vingi kwa kiasi kikubwa Tanzania tunasifika kuwa na vivutio vya asilia mbapo hiyo ni bidhaa ya kwanza, ya pili hatujawai sana kutumia maji kama mazao ya utalii, kuanzisha sakta hii ya utalii kwa ukanda huu ya kutumia ziwa Victoria na Tanganyika maana yake tunatoa fursa ya watu kuona nini ni wanaweza wakafanya kupitia maziwa haya,linaweza kuwa zao la pili ambalo linaweza kutusaidia kuleta upekee katika ukanda huu,eneo la tatu ni  mila na desturi za watu wa maeneo haya,kabila yaliyopo hapa ni mengi  mfano Mkoa wa Mara una zaidi ya makabila 16 ambapo una kuta kijiji kimoja kabila hili kijiji kingine kabila jingine,pia kabila hili la wasukuma,tuna madini ya dhahabu na almasi,”alisema Dkt.Kigwagala.

Aidha alisema,ni jambo la msingi kwa hatua hiyo ya awali kwa ukanda huo kuzitambulisha fursa zilizopo ili zijulikane na kusaidia uelewa wa vivutio ili kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza na kuandaa miundombinu ya utalii ambapo ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi(CCM) ya mwaka 2015-2020 inazungumzia suala la kukuza utaliii na ielekeza wizara husika kuongeza watalii kutoka milioni 1 mwaka 2015 hadi milioni 2 mwaka huu.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Prof. Adolf  Mkenda, alisema maonesho hayo yanatarajiwa kuwa na washiriki kutoka nchi mbalimbali duniani zenye vivutio  zitapenda kuja  kutangaza vivutio vyao nchini hapa.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii Nchini {TBB} Jaji Mstaafu Thomas Mihayo, alisema bodi hiyo ipo tayari kusimamia,kujitolea na kushughulika ili maonesho hayo ambayo ni ya  kwanza na ya aina yake yaweze kufanikiwa na kufanyika kwa ngazi ya kimataifa huku akiwahimiza wakuu wa mikoa hiyo inayohusika katika maonesho hayo kutangaza shughuli hiyo kila mara kuwa itafanyika mkoani Mwanza pamoja na watendaji wasekta hiyo wakijipange katika ufanyaji kazi.

Baadhi ya wakuu wa mikoa itakayoshiriki katika maonesho hayo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella na Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Gabriel wamesema wapo tayari kushirikiana kwa pamoja ili kuweza kuibua na kuendeleza fursa za utalii zinazopatikana huku Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Emmanuel Maganga akitumia fursa hiyo kutoa ombi la kupatika naeneo  la kudumu kwa ajili ya kufanyia maonesho hayo.

“Sisi kama Mikoa tupo tayari tumejipanga kwa fursa zilizopo katika mikoa yetu,ili kuweza kushiriki katika matayarisho, lakini vilevile kuhamasisha wadau kutoka sekta mbalimbalia mbao ni wadau katika sekta ya utalii kushiriki kama ambavyo inatarajiwa mwisho wasiku  kutoa mchango wa kutosha kwa maendeleo ya mikoa yetu,watu wetu na nchi yetu kwa ujumla,”alisema Mhe.Mongella.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.