• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MACHINGA MKOA WA MWANZA HATUTAANDAMANA : MWENYEKITI SHIUMA

Posted on: January 22nd, 2024

MACHINGA MKOA WA MWANZA HATUTAANDAMANA : MWENYEKITI SHIUMA


Mwenyekiti wa Shirikisho la Umoja wa Machinga Mkoa wa Mwanza (CHIUMA) Mohamed Dauda amesema wafanyabiashara wadogo Mkoa huo (Machinga) hawataandamana Janauri 24, 2024 kama inavyohamasishwa na vyama vya siasa.

Dauda ametoa tamko hilo mapema leo tarehe 22, Januari 2024 wakati wa mkutano wa shirikisho hilo pamoja na waandishi wa Habari uliofanyika kwenye Stendi ya Mabasi Nyegezi.

Amesema, kundi hilo linalojipatia kipato kupitia biashara ndogondogo halipo tayari kutumiwa na wanasiasa kwani wataathiri biashara zao kwa kujihusisha na uvunjifu wa amani.

Amesema kundi hilo wanamshukuru Rais Samia kwa kuwawekea mazingira rafiki ya kazi kwa kuwajengea Ofisi nchi nzima na kuwatengea maeneo na kwamba imekua ni fursa sahihi ya kukuza kipato na uchumi wa nchi kwa ujumla.

Ameendelea kufafanua kwamba hakuna machinga atakayeandamana mkoa mzima na yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua za kinidhamu ikiwemo kuondolewa kwenye shirikisho lao mara moja.

Katibu Mkuu wa shirikisho hilo Venatus Anatory ametumia wasaa huo kuhamasisha bodaboda kujikinga na janga la Kipindupindu na akatoa wito kwao kuweka vibeba taka kwenye maeneo yao na kuhakikisha wananawa maji tiririka.

"Hoja zetu na Serikali ya Rais Samia zinaishia mezani, hatuna sababu ya kuandamana maana hata tulipokutana naye Dodoma alitusikiliza na tuna furaha kwani tunafanya biashara kwa uhuru hatubughudhiwi na mtu." Katibu Mkuu.

Naye Beatrice Mgema, mfanyabiashara kwenye Stendi ya Nyegezi amebainisha kuwa Rais Samia ni kama mlezi wa biashara zao kwani amewawekea mazingira mazuri ya kazi na kwamba riziki wapatazo hawako tayari kuharibu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.