• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MADAKTARI BINGWA KUWEKA KAMBI YA MATIBABU SIKU 5 MWANZA

Posted on: October 20th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amepokea madaktari bingwa na bobezi 58 wa Mama Samia wa awamu ya nne kutoka katika kada sita ambao wamekuja kuweka kambi za matibabu katika Hospitali za Wilaya na Halmashauri 8 za Mkoa huo.

Madaktari hao wataweka kambi Mkoani Mwanza kuanzia tarehe 20 hadi 24 Oktoba 2025 wakitarajiwa kutoa huduma za Ubingwa katika maeneo ya magonjwa ya ndani, wanawake na ukunga, upasuaji, ubobezi kwa watoto wachanga, ubingwa katika huduma za kinywa na meno, usingizi na ganzi, pamoja na huduma za ubingwa na ubobezi katika uuguzi.

 

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kambi hiyo Bw. Balandya amesema ujio wa madaktari hao bingwa ni wa faida kwa watumishi wa idara ya afya pamoja na wananchi kwani utasaidia katika kutoa elimu, mafunzo na huduma.

“Naamini kwamba ujio wenu katika Mkoa wa Mwanza utasaidia kukuza ujuzi wa hawa wenzetu waliopo katika Mkoa huu ili waweze kuondokana au kupunguza changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao ya kazi”. Amesema Bw. Balandya.

Aidha, amewahakikishia wataalamu hao kupata ushirikiano kutoka ngazi ya Mkoa na Halmashauri kwa kipindi chote ambacho watakua wameweka kambi Mkoani humo, huku akiwakaribisha wananchi wa Mkoa huo kujitokeza kwa wingi kupatiwa matibabu.

Vilevile, Katibu Tawala ametumia wasaa huo kuishukuru serikali kwa kuwaletea wataalamu hao huku akibainisha kuwa mara zote imekua ikihakikisha inaboresha huduma na miundombinu mkoani humo na akazitaja Bilioni 63 zilizotolewa kwa ajili ya kuboresha miundombinu na vifaa tiba kwa kipindi cha miaka 4.

Naye, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewasisitiza madaktari hao bingwa kwenda kubadilishana ujuzi na madaktari ambao watawakuta katika hospitali za Wilaya.

Msimamizi wa timu hiyo kutoka Wizara ya Afya Bi. Fidea Obimbo amesema lengo kubwa la kambi ya madaktari bingwa na bobezi kufika Mkoani Mwanza ni kuwafikia wananchi kwa huduma tofauti ambazo zilikua ni ngumu kwao kuwafikia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA KUWEKA KAMBI YA MATIBABU SIKU 5 MWANZA

    October 20, 2025
  • TUME YA MIPANGO YAENDELEA KUTOA MAFUNZO YA DIRA YA TAIFA YA MAENDELEO 2050 KWA TAASISI BINAFSI

    October 09, 2025
  • E-MABORESHO IMEKUJA KIMKAKATI KUMALIZA RUSHWA NCHINI- RAS BALANDYA

    October 09, 2025
  • WAZEE ZINGATIENI LISHE BORA KUJIKINGA NA MARADHI - RC MTANDA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.