• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Madereva waomba sheria izingatie pande zote mbili

Posted on: August 29th, 2019


Chama cha Madereva Mkoa wa Mwanza na kile cha Wamiliki wa Mabasi (TABOA) kwa pamoja wameiomba serikali kutunga na kutilia mkazo kanuni na sheria zitakazowabana abiria ambao hawafuati sheria za barabarani.

Hayo yamesemwa  mkoani Mwanza katika mkutano ulioandaliwa na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) uliolenga kukusanya maoni kutoka kwa wadau mbalimbali wa usafirishaji juu ya rasimu mpya ya kanuni na sheria za sekta hiyo nchini.

Akizungumuza kwa niaba ya wanachama wa chama cha madereva Mkoa wa Mwanza Salim Iddy, alisema kwa muda mrefu sasa sheria na kanuni za usalama barabarani zinazotungwa zimekuwa zikilenga zaidi kuwabana madereva huku zikiwaacha abiria wakifanya wanavyotaka.

“Kuna wakati unakuta abiria wanapanda kwenye mabasi wakiwa wamelewa au hata na chupa za vilevi wanakuwa wasumbufu toka mwanzo hadi mwisho wa safari, kiasi cha kusababisha dereva kuendesha bila amani na hata kumfanya apoteze umakini wakati wa safari.

“Pia wapo abiria wanapenda kusimama maeneo yasiyokuwa na vituo vya daladala lakini dereva anapowachukua yeye ndiyo anapigwa faini, tunaziomba mamlaka zinazohusika ziwachukulie na wao hatua kwani wao ndiyo chanzo cha uvunjifu wa sheria za barabarani,” alisema Iddy.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha wamiliki wa mabasi Mkoa wa Mwanza, Anwar Said, aliongeza kuwa kuna haja ya serikali na vyombo vinavyohusika kuanza kuvibana kwanza vyombo vya usafiri vya umma ikiwemo mabasi ya mwendo kasi ili kuonyesha mfano kwa wengine.

“Suala la kudhibiti uzidishwaji wa abiria kwenye vyombo vya usafiri limekuwa likilenga zaidi mabasi yanayomilikiwa na watu binafsi, serikali inatakiwa ianze na mabasi ya mwendo kasi ambayo yanabeba abiria kupita kiwango.

“Pia waendeshaji wa magari ya serikali mara nyingi wanatumia mwendo mkubwa kuliko kawaida lakini cha kushangaza hakuna hatua zinazochukuliwa huku madereva wetu wakizidisha mwendo kidogo tu mnawakamata mnawapiga faini, huo ni uonevu kwa kuwa sheria ni zetu sote.

“Hivi sasa pia tunashuhudia ongezeko na utitiri wa mamlaka zinazodhibiti vyombo vya usafiri nchini tunaiomba serikali iliangalie hili na kama itawezekana zipunguzwe, kwani kadri mamlaka zinavyozidi kuwa nyingi ndio mianya ya rushwa inaongezeka kutoka kwa madereva na wafanyakazi wetu, alisema Anwar.







Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.