• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Maonesho ya Nanene mwaka huu Mwanza yaje na matokeo chanya katika kilimo-RAS

Posted on: August 2nd, 2023


Wadau wa Kilimo na wajasiriamali kwa ujumla katika sekta ya hiyo wameaswa kuyatumia maonesho ya Nanenane mwaka huu Mwanza kuja na matokeo chanya kwa kufanya shughuli zao kisasa zaidi na kuwa na tija.

Akizungumza leo maeneo ya Nyamhongolo  mara baada ya kukagua maandalizi ya maonesho hayo yatakayo zinduliwa rasmi kesho,Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu,Ndg. Daniel Machunda aliyemuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza amesema maonesho ya mwaka huu yataambatana na fursa za kuelimishwa namna ya kufanya shughuli kuanzia za Kilimo kwa kisasa zaidi na jinsi ya kukabiliana na changamoto zake.

"Nimefarijika kwanza kwa hamasa ya watu kujitokeza kwa wingi,nimejionea shughuli mbalimbali za wadau na hasa Taasisi za kifedha zilizojitokeza kuonesha huduma zao ikiwemo Benki Kuu ya Tanzania," amesema Machunda.


"Tupo hapa kwa lengo la kuwajengea uwezo wadau na wananchi kwa ujumla kuhusu huduma zetu na utambuzi sahihi wa fedha zetu hasa kutokana na ulaghai wa fedha bandia uliopo sasa hivi,wapo wataalamu mbalimbali kwenye banda letu watakao toa ufafanuzi mbalimbali,"Issa Pagali,msimamizi banda la BoT

"Tunashukuru tena kupata fursa hii,Serikali yetu imeweka mkakati mzuri wa mageuzi katika kilimo kuanzia ufugaji wa kisasa na wenye tija,nina mifugo yangu ambayo sasa inanipa faida kutokana na maonesho haya ya Nanenane baada ya kukutana na wataalamu walionielimisha," Elizabeth Masatu,mkulima.

Mratibu wa Maonesho hayo Kanda ya Ziwa

Magharibi,Peter Kasele amebainisha maandalizi yote yamekamilika kuanzia maboresho ya mazingira na usalama kwa muda wote wa Maonesho hayo yatakayo zinduliwa rasmi  alhamisi hii na wale walio mbali na Mwanza watayashuhudia mubashara kupitia luninga ya Star Tv.

Maonesho ya Nanenane yanayofanyika kila mwaka Mwezi Agosti yanaandaliwa kwa kushirikisha Mikoa ya Mwanza kama wenyeji pamoja na Geita na Kagera wanaounda Kanda ya ziwa Magharibi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.