• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mapato, uchumi vyaimarika Mwanza

Posted on: March 22nd, 2020

Maendeleo ni mchakato mrefu unaogharimu muda, rasilimali fedha na utaalam.

Kote duniani maendeleo hupimwa katika misingi ya kuimarika na kuboreka kwa huduma za kijamii.

Ili kufikia maendeleo, ni lazima pawepo mikakati madhubuti na endelevu ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati ya muda mfupi, kati na mrefu.

Tangu ilivyoingia madarakani Novemba 5, 2015, Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais John Magufuli imejipambanua kuwa na nia thabiti ya kujenga Tanzania mpya, Tanzania ya watu wanaochapa kazi.

Katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wake, Rais Magufuli amefanya mengi ya kupigiwa mfano katika maendeleo ya sekta za afya, elimu, maji, usafirishaji, na miundombinu ya barabara.

Kazi zote zimefanyika kutekeleza ilani ya uchaguzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ahadi za Rais Magufuli wakati wa kampeni za uchaguzi mwaka 2015 pamoja na ahadi au mahitaji mengine yanayotokea katika ziara mbalimbali za viongozi.

Kwa mkoa wa Mwanza, kazi nyingi na kubwa zimefanyika kuhakikisha upatikanaji wa maendeleo endelevu kwa wananchi.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongela anasema mikakati hiyo ya maendeleo inahusisha mazingira wezeshi kwa wananchi kufanya na kushiriki shughuli za uzalishaji mali kuanzia ngazi ya msingi hadi Taifa.

“Tunapozungumzia Tanzania yenye uchumi wa kati kupitia maendeleo ya sekta ya viwanda ifikapo 2015, tunalenga kumwezesha kila Mtanzania pale alipo kuzalisha, kuuza na kufanya biashara kulingana na mahitaji, mazingira na mtaji wake,” anasema Mongella

Sekta za kilimo, uvuvi, uwekezaji na biashara ni kati ya maeneo muhimu yanayotumiwa na wakazi wa mkoa wa Mwanza kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

Shughuli mbalimbali za kiuchumi zinazotekelezwa na wakazi wa mkoa huo umewezesha mkoa wa Mwanza kushuhudia ukuaji wa uchumi kwa kwa asilimia 8 huku pato la mkoa likiongezeka kila mwaka.

Mongella anasema kwa mujibu wa takwimu za Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Pato la Mkoa wa Mwanza limeongezeka kutoka Sh10.05 trilioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh11.3 trilioni mwaka 2017.

Kiwango hicho kimeufanya mkoa wa Mwanza kushika nafasi ya pili baada ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Mkoa pia umeshika nafasi ya pili Kitaifa kwa kuchangia asilimia 9.79 ya pato la Taifa mwaka 2017 kulinganisha na asilimia 9.69 ya mwaka 2016.

“Wastani wa kipato kwa mwaka kwa kila mwananchi umeongezeka kutoka Sh2.2 milioni mwaka 2016 hadi kufikia Sh2.3 milioni mwaka 2017.

“Ongezeko la kipato inaimarisha uwezo wa wananchi wa kununua na kuuza; hii inatoa ishara njema kwa uchumi wa mkoa na mtu mmoja mmoja,” anasema Mhe.Mongella.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.