• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NI MUHIMU KWA KUPANGA MIRADI NA HUDUMA KWA JAMII-RC MAKALLA

Posted on: October 13th, 2023

MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI NI MUHIMU KWA KUPANGA MIRADI NA HUDUMA KWA JAMII-RC MAKALLA.


*Ampongeza Rais Samia kwa kufanikisha Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022*


*Asisisitiza makundi ya vijana yaelimishwe ili watambue fursa za kiuchumi zilizopo maeneo yao*


*Ashauri mipango imara ifanyike ya huduma zote za msingi kwa wananchi na kuondoa umasikini wa kipato*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Makalla amesisitiza kuwepo na kipaumbele wa utoaji elimu ya matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa makundi ya vijana ambao ndiyo nguvu kazi ya Taifa ili watambue fursa za kiuchumi zilizopo maeneo yao.

Akifungua leo Oktoba 13, 2023 Mafunzo ya matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mhe Makalla amesema makundi ya vijana wakipata elimu ya kutosha itawasaidia kujikomboa kiuchumi kwa kutumia vizuri fursa zinazowazunguka.

"Kuna kasumba ya kundi la vijana kupenda kukimbilia maeneo ya mjini kutafuta kazi mbalimbali na kujikuta wakiwacha fursa za kiuchumi zilizopo maeneo yao, hivyo kwa kupitia elimu watakayopata itawafumbua macho na kujipatia kipato," CPA Makalla.

Aidha, amebainisha kuwa kwa Mkoa wa Mwanza takwimu zinaonesha kuna idadi ya watu milioni 3.7 huku Halmashauri ya Nyamagana ikiongoza kwa idadi kubwa ya watu, hivyo ni wajibu kwa wahusika kuja na mipango kuanzia ngazi ya chini.

"Hivi sasa nimeanza kusikiliza kero za wananchi, nashuhudia kundi kubwa la vijana wakilalamikia kukosa kazi na kuomba nafasi mbalimbali kwenye majeshi yetu,hii inadhihirisha bado kuna jambo la msingi la kuwasaidia", amesisitiza Mhe.Makalla wakati akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo.

Vilevile, amemshukuru Rais  Mhe. Dkt. Samia Suluhu kwa kufanikisha Sensa ya watu na makazi kwa kutoa vishkwambi vilivyotumika nchi nzima vilivyossidia kazi ya Sensa kufanyika kwa ubora na umakini.

Awali akizungumzia malengo ya mafunzo hayo Afisa kutoka Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Benedict Mugambi amebainisha malenngo ya Sensa ni Serikali kupata hesabu halisi ya wananchi wake ili iweze kuweka mipango imara ya kuwahudumia kulingana na maeneo wanayoishi,hivyo wananchi pia wana wajibu wa kutumia vizuri matokeo hayo ili kuweza kujiinua kiuchumi.

"Tumetoa mafunzo haya kwa Wilaya za Nyamagana na Ilemela na leo tunatoa ngazi ya Mkoa,lengo ni kuja na matokeo chanya kwa kuona namna ya kutoa huduma bora kwa wananchi na pia fursa za kiuchumi zilizopo maeneo husika,"Benedict Mugambi, Meneja Idara ya shughuli za kitakwinu.

Kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022, Tanzania Ina jumla ya watu milioni 61.7 huku Mkoa wa Njombe ukiwa na idadi ndogo ya watu 900,000 na kwa upande wa Zanzibar Mkoa wa kusini Unguja ukiwa na idadi ndogo ya watu 200,000.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.