• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MELI YA MV. MWANZA YAPOKEA SHEHENA ZA SAMANI

Posted on: March 24th, 2025

MELI YA MV. MWANZA YAPOKEA SHEHENA ZA SAMANI


Leo Machi 24, 2025 Mkuu wa Wilaya  Nyamagana Mhe. Amina Makilagi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ameongoza hafla fupi ya mapokezi ya magari tisa yaliyobeba makasha yenye mzigo wa samani zitakazofungwa kwenye Meli ya Mv. Mwanza inayojengwa katika ziwa Viktoria.

Akizungumza katika mapokezi hayo Mhe. Makilagi amesema kuwasili kwa samani hizo ni hatua muhimu katika kuelekea kukamilisha mradi huo ambao kwa sasa umefikia asilimia 96 ya utekelezaji wake na ambao unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Mei, 2025.

“Hatua hii ya mwisho ni kielelezo tosha ya namna Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alivyoufungua Mkoa wa Mwanza, unao changia pato la Taifa kwa asilimia 7.2”. Mhe. Makilagi.

Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya ameitaka Menejimenti ya Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) kuhakikisha inasimamia vema mradi huo ili ukamilike kama ulivyopangwa na kufanikisha azma ya Serikali ya kuboresha huduma ya usafiri kwa njia ya maji kwa abiria na mizigo kwa wananchi wa Kanda ya Ziwa.

“Kukamilika kwa mradi huu kunatarajiwa kuongeza chachu kwa ukuaji wa uchumi kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa na nchi jirani kwa kutoa huduma za usafiri zilizo salama, bora na za uhakika”. Amesema Mhe. Makilagi

Naye, Kaimu Mkurugenzi wa TASHICO Bi. Amina Mtibampema amesema leo wamepokea vifaa yaani viti vya madaraja yote ambapo mara baada ya kukamilika kwa zoezi la umaliziaji wa meli hiyo kampuni hiyo ya meli itakwenda kufungua uchumi wa Mkoa, wafanyakazi wa TASHICO pamoja na Taifa kiujumla.

“Tutaendelea kusimamia mradi huu kwa maendeleo ya Taifa, na baada ya kupokea Vifaa hivi ufungaji utaanza mara moja”. Bi. Amina.

Mradi huo wa Meli ya Mv. Mwanza kwa sasa umefika asilimia 96 na fedha zilizolipwa hadi sasa ni asilimia 93. Aidha Meli hiyo itakapokamilika itakuwa ndiyo meli kubwa kuliko zote katika Ziwa Viktoria ikiwa na uwezo wa kubeba abiria 1,200, tani 400 za mizigo, magari madogo 20 na magari makubwa 3.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.