• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MHE. MAJALIWA ATAKA SEKTA MTAMBUKA KUWEKA MSINGI MATHUBUTI KUIMARISHA LISHE NCHINI

Posted on: October 3rd, 2024

MHE. MAJALIWA ATAKA SEKTA MTAMBUKA KUWEKA MSINGI MATHUBUTI KUIMARISHA LISHE NCHINI


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (MB) amezitaka sekta mtambuka kushirikiana katika kutekeleza afua za lishe ili kuondoa tatizo la utapiamlo, udumavu na ukondefu nchini.

Mhe. Majaliwa amesema ni lazima wizara za kisekta kama za Elimu, TAMISEMI, Kilimo, Uvuvi, Maendeleo ya jamii na Afya kushirikiana na wadau katika kuweka mikakati na mipango itakayosaidia kutekeleza sera na msingi mathubuti wa lishe nchini.

Mhe. Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo Alhamisi Oktoba 04

., 2024 katika Mkutano Mkuu wa kumi wa wadau wa lishe uliofanyika katika ukumbi wa hoteli ya Malaika beach resort Wilayani Ilemela Mkoani Mwanza.

Aidha, amesema Serikali inaendelea  kutokomeza aina zote za utapiamlo nchini ikiwemo kutekeleza mkakati wa kuimarisha lishe bora, kuajiri wataalamu wa lishe na kusaini mikataba na viongozi wa Mikoa na Wilaya ya kutekeleza afua za lishe.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Mkoa huo unaendelea kutekeleza afua za lishe na mikakati yote ya kuweka jamii kwenye afya bora na kuwatoa wananchi kwenye utapiamlo, unyongefu na udumavu wa akili na mwili.

Aidha, ametumia wasaa huo kuwaalika wadau kwenye maadhimisho ya kilele cha mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa kitakachofanyika   Oktoba 14, 2024 kwenye uwanja wa CCM Kirumba ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania.

Kwa upande wake Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bw. Jimmy Yonazi amesema mkutano huo umeweka maazimio kadhaa yakiwemo ombi kwa Serikali kujumuisha masuala ya Lishe kwenye dira ya Taifa 2050, kuratibu na kuteleza masuala ya lishe kwa kipaumbele pamoja na kuimarisha sekta binafsi ili zishiriki kwenye masuala ya lishe.

Mkutano huo wa siku mbili umefanyika chini ya kaulimbiu isemayo; "Kuchagiza mchango wa wadau wa kisekta ili kudumisha matokeo bora ya hali ya lishe nchini Tanzania".

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.