• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Michezo ya UMITASHUMTA yazinduliwa rasmi Mwanza

Posted on: July 20th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amewataka wanafunzi Kujituma, kuweka bidii ya kizalendo na kufuata Sheria na Taratibu za Michezo ili kupata wanamichezo bora watakaouwakilisha Mkoa kwenye michezo ya UMITASHUMTA Kitaifa Mkoani Tabora mwishoni mwa mwezi.

Ametoa wito huo leo Julai 19, 2022 wakati akifungua Michezo ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi Tanzania (UMITASHUMTA) inayowakutanisha wanafunzi 660 kutoka Halmashauri 8 za Mkoa wa Mwanza wanaoshiriki michezo hiyo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Nsumba.

"Wachezaji mliochaguliwa kushiriki michuano ya Mkoa mnapaswa kujituma ili muweze kufuzu michuano ya Mkoa, Kitaifa na hata badae ya kimataifa kwani vipaji ni ajira na biashara hivyo zingatieni yote ili mtimize ndoto zenu." Amesema.

Martin Nkwabi, Afisa Elimu Mkoa amesema kuwa kwenye mfumo wa Elimu kuna uhusiano mkubwa sana kati ya elimu na michezo na ndio maana sehemu ambayo michezo imeimarika watoto wanafaulu zaidi kwakua afya ya mwili inafungua akili vizuri zaidi.


Amefafanua kuwa michezo husaidia kufuta ubaguzi wa makabila, elimu, rangi na kufanya watu kuwa wamoja na wenye mshikamano kwani kinachozingatiwa ni umahiri tu uwanjani bila kujali ni nani ameonesha kipaji hicho.


 Joseph Mambo, Mratibu wa UMITASHUMTA Mkoa wa Mwanza 2022 amebainisha kuwa mashindano hayo ngazi ya Mkoa yatadumu kwa siku tano na watakaofuzu watauwakilisha Mkoa Kitaifa Mkoani Tabora mwishoni mwa Mwezi Julai mwaka huu.


Vilevile, amefafanua kuwa mashindano hayo muhimu yatahusisha pia wanafunzi kutoka makundi maalumu yatasaidia kuwaunganisha vijana wa Tanzania kitaifa, kupanua wigo wa ufahamu wa watoto kijiografia na kuibua vipaji na taaluma kwa watoto ni miongoni na taaluma.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.