• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MILIONI 92.2 ZA MAPATO YA NDANI KUPUNGUZA VIFO VYA UZAZI NYASHIMBA-MAGU

Posted on: August 27th, 2025

Mwenge wa Uhuru leo Agosti 27, 2025 umezindua Zahanati katika kijiji cha Nyashimba wilayani Magu iliyojengwa kwa Tshs. Milioni 92.2 kutoka chanzo cha makusanyo ya mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Akizungumza na maelfu ya wananchi waliojitokeza kuipokea zahanati hiyo, Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru Kitaifa 2025 Bw. Ismail Ali Ussi amewapongeza Viongozi wa Halmashauri na Wilaya hiyo kwa kutoa fedha ambapo amesema zitasaidia kuboresha huduma hususani za mama na mtoto na kupelekea kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

Aidha, amewapongeza wananchi kwa kuchangia nguvu kazi kwa zaidi ya Tshs. Milioni 16 kwani wameonesha uzalendo na kiu ya kupata huduma bora za afya jirani na makazi yao na kupelekea kuukwamua mradi huo uliochelewa tangu mwezi Januari, 2018 hadi ilipokamilika mwezi Agosti, 2025.

Aidha, Mwenge wa uhuru umeleta neema kwa wananchi wa kijiji cha Njicha-Ihayabuyaga kwa kuwazindulia mradi wa maji uliogharimu zaidi ya Milioni 256 zilizotolewa na Shirika la Lotary Club (SLC) unaozalisha lita elfu 5 kwa saa ambao umeinua hali ya upatikanaji wa maji safi kutoka 37% hadi 74 kwa wakazi wa eneo hilo.

Akizindua mradi huo, Kiongozi wa mbio za Mwenge amewapongeza Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kwa kujenga mradi huo na kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya faida ya mradi na kupelekea kutoa eneo la ujenzi bure pamoja na kuchangia nguvu kazi.

Mradi huo wa maji unahudumia wananchi zaidi ya 4500 ambao ni sawa na asilimia 75 ya wakazi wote katika kijiji hicho ambao una miundombinu kama visima 2, matenki 6, minara 2, mtandao wa bomba pamoja na sehemu za kuchotea maji.

Mradi wa vijana waosha magazi waliokopeshwa milioni 30 na halmashauri umefungua dimba kwa mbio za mwenge wa uhuru wilayani humo kabla ya kukagua miundombinu ya Nishati Safi ya kupikia katika shule ya sekondari ya wasichana yenye thamani ya Milioni 13 na kuhitimisha kwa kuzindua barabara ya RC Hostel mjini Magu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KIONGOZI MBIO ZA MWENGE AIPONGEZA KWIMBA KUONGEZA WIGO UKUSANYAJI MAPATO

    August 28, 2025
  • RAS BALANDYA AWATAKA MAAFISA USAFIRISHAJI KUBORESHA HUDUMA ZAO

    August 28, 2025
  • WANANCHI 8488 KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA MALIGISU KWIMBA

    August 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAANZA MBIO ZAKE KWIMBA

    August 28, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.