• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MKATABA WA UJENZI WA JENGO LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE MWANZA WASAINIWA RASMI

Posted on: March 28th, 2024
  1. MKATABA WA UJENZI WA JENGO LA ABIRIA UWANJA WA NDEGE MWANZA WASAINIWA RASMI


*Prof. Mbarawa mgeni rasmi kwenye hafla ya kusaini mkataba huo*


*RC Makalla asema Rais Samia anastahili pongezi ameweka hostoria kanda ya ziwa*


*RC Makalla asema usafirishaji minofu ya samaki, na utalii utakuzwa*


Leo Machi 28, 2024 historia imeandikwa kwenye Viwanja vya Jengo la mizigo (Cargo Terminal) la uwanja wa ndege wa Mwanza kwa kusainiwa rasmi mkataba wenye thamani ya Bilioni 29 kwa ajili ya ukamilishaji wa jengo la kisasa la abiria katika uwanja wa ndege wa Mwanza.

Akiongea na wananchi, mgeni rasmi wa hafla hiyo Mhe. Prof. Makame Mbarawa (MB) Waziri wa Uchukuzi amesema Serikali imeendelea kuboresha viwanja mbalimbali vya ndege nchini na kwamba zaidi ya Shs. Trilioni 1.1 zimetumika na kwamba ana imani kubwa na Mamlaka ya viwanja vya ndege,TAA wanaosimamia kazi hizo.

Aidha, Prof. Mbarawa amewataka mamlaka hiyo kuwekeza kibiashara kwenye viwanja vya ndege ili miundombinu inayojengwa isaidie kuinua uchumi wa nchi na akatumia wasaa huo kubainisha kuwa uwanja wa ndege wa Bukoba uko salama na ndege zinatua na kuondoka wakati wote.

Akitoa salamu za Mkoa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amemshukuru Rais Samia kwa kukubali pendekezo la kukabidhi ujenzi huo kwa Mamlaka ya Viwanja vya ndege ili liweze kukamilika kwa kasi na amempongeza kwa kuweka historia katika utekelezaji wa miradi kanda ya ziwa.

Aidha, amebainisha kuwa uwepo wa jengo hilo lenye uwezo wa kuchukua abiria 600 kwa wakati mmoja pamoja na upanuzi wa uwanja vitakuza utalii pamoja na kusaidia kusafirisha minofu ya samaki na mizigo mingine kutokea Mwanza moja kwa moja pamoja na kusaidia kukuza Utalii.

"Baada ya hili jengo kukamilika pamoja na miradi mingine inayojengwa Mkoani kwetu kama ule mradi wa SGR, Mwanza itakua na fursa kubwa sana kwa uwekezaji hivyo ni lazima wananchi tujiandae na neema hizo." Mhe. Michael Masanja, Mwenyekiti CCM Mkoa.


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) Bw. Musa Mbura amebainisha kuwa kuanzia mwaka 2020 serikali imeendelea kufanya maboresho ya uwanja huo ikiwemo upanuzi wa barabara ya kutua na kupaa, ujenzi wa jengo la mizigo, kituo cha taarifa za hali ya hewa pamoja na jengo na mifumo ya kuongozea ndege.


Ameongeza kuwa mwaka 2024/25 Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) itafanya maboresho ndani ya muda mfupi ikihusisha eneo la biashara, eneo la Maegesho, barabara ya kuingia na kutoka kwenye jengo hilo, barabara kiunganishi kwenda kwenye ndege na kwamba ndani ya miezi 10 litakamilika chini ya Mkandarasi mzawa Taifa Mining and Civil LTD.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.