• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkoa wa Mwanza wajizatiti kupunguza ajali za barabarani

Posted on: March 14th, 2023


Wakati Watanzania wengi wakipoteza maisha, kupata majeraha na ulemavu wa kudumu kutokana na ajali za barabarani, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amesema wamejipanga kupunguza ajali hizo kwa kuchukua hatua na kuweka mikakati mbalimbali ikiwamo   kuwahamasisha bodaboda  kufuata alama na ishara zinazotolewa na wasimamizi wa sheria.

Mhe.Malima ameyasema hayo leo Machi 13, 2023 jijini Mwanza wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kuhusu maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani kitaifa inayofanyika mkoani hapa kuanzia Machi 14 hadi 17 huku Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa akiwa mgeni rasmi ambapo kauli mbiu ni 'Tanzania bila ajali inawezekana - Timiza wajibu wako'.

Mhe.Malima amesema kwa kipindi cha Januari - Desemba, 2022 jumla ya ajali kubwa 81 zimeripotiwa, zilizosababisha vifo vya watu 71 na majeruhi 96, huku ajali za pikipiki pekee zikiwa 30 zilizosababisha vifo vya watu 25 na kujeruhi 26 ambapo ameeleza kwamba mwelekeo wa takwimu hizo siyo mzuri na kuwataka watumia barabara kuzingatia sheria ikiwamo kuacha mwendokasi, ulevi, kujaza abiria na mizigo kupita kiasi na ubovu wa vyombo vya moto.

Amewataka watumiaji wa barabara mkoani hapa kukagua vyombo vya moto mara kwa mara ili kuepusha ajali zinazotokana na ubovu wa vyombo hivyo, huku akisisitiza kutoegesha barabarani kwa zaidi ya saa mbili magari mabovu yaliyoharibika.

"Mwanza tuna kauli mbiu ya kudumu kuhusu usalama barabarani inayosema 'karibu mkoa wa Mwanza:- tafadhali zingatia sheria na kanuni za usalama barabarani, epuka adhabu kali'," amesema Mhe. Malima.

Vile vile, Mhe. Malima amewataka abiria kutoshabikia vitendo vya ukiukwaji wa sheria ikiwamo mwendokasi bali wakemee na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi wanapoona ukiukwaji huo.

"Wananchi walio kandokando ya barabara wasijichukulie sheria mkononi inapotokea ajali katika maeneo yao ikiwa ni pamoja na kuepuka kuchoma matairi na kuweka magogo kwa nia ya kufunga barabara kwa sababu hali hiyo huleta usumbufu kwa watumiaji wengine wa barabara ambao wana matatizo mbalimbali," amesema Mhe. Malima.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.