• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mkuu wa Mkoa Mwanza ahimiza huduma za maji kwenye Vituo vya kutolea huduma za afya/elimu

Posted on: March 2nd, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ameziagiza Halmashauri na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) kushirikiana kupeleka Maji safi na salama kwenye vituo vyote vya kutolea huduma za afya pamoja na taasisi za Elimu mkoani humo ili kupunguza adha kwa watumishi na wananchi wanaopata huduma.

Akikaguzi Maendeleo ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Buzilasoga wilayani Sengerema unaotarajia kuwahudumia zaidi ya wananchi 1852 chini ya Mpango wa kunusuru Kaya Masikini (TASAF III) kwa zaidi ya Milioni 543, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema huduma za Afya haziwezi kutolewa pasipo kuwa na Maji ya kutosha.

Amesema pamoja na fedha za Mradi huo kuhusisha Ujenzi wa Miundombinu kama vile Wodi ya Wazazi, Watoto, Maabara na Jengo la Kupokelea wagonjwa wa nje ni lazima Halmashauri na RUWASA kushirikiana kutafuta fedha za kuchimba kisima kirefu cha maji mara moja kabla ya kuanza kwa kutoa huduma.

"Kituo cha Afya bila huduma za Maji haiwezekani na tusidanganyane na kutegemea chanzo cha maji ya mvua badala yake naomba Halmashauri itenge angalau Milioni 30 hapa ili tupate kisima  kirefu cha maji kwenye kituo hiki." Amesema Malima.

Aidha, ameagiza Halmashauri hiyo kuongeza muda wa kufanya kazi na Rasilimaliwatu ili hadi kufikia Machi 15, 2023 mradi huo uwe umekamilika na ili kuweza kutimiza vigezo vya kuendelea kupata ufadhili wa miradi mingine ya maendeleo.

Naye, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Balandya Elikana amewataka wananchi wa kijiji cha Mami kilichopo kata ya Kishinda kuendelea kujitolea nguvu kazi kwenye mradi ya Maji wa Zahanati ya Kijiji ambapo Mkuu wa Mkoa amechangia Shilingi Laki 5 kuunga mkono juhudi za wanamchi wanaochimba mtaro wa Maji.

"Mhe. Mkuu wa Mkuu, Mradi huu umefikia Asilimia 80 ya Ujenzi na tunatarajia kuukamilisha baada ya wiki moja" Amesema Ndugu. Malisa Nguda, Mratibu wa TASAF Wilaya ya Sengerema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.