• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mongella apokea vifaa vya kujikinga na Corona Mwanza

Posted on: April 16th, 2020


Wadau wa Maendeleo na Taasisi mbalimbali za maendeleo zimetoa vifaa mbalimbali vikiwemo meza, ndoo, sabuni, diaba na matenki ya maji kwa ajili ya kusaidia kwenye mapambano ya Corona.

Vifaa hivyo vimepokelewa  jijini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe.John Mongella ambaye amezishukuru taasisi hizo na wadau hao wa maendeleo kwa moyo wa kujitoa katika kuunga mkono juhudi za Serikali kwenye mapambano ya ugonjwa wa homa ya mapafu( Corona) ambalo kwa sasa ni janga la dunia.

Aidha Mhe.Mongella amewataka wadau hao wa maendeleo kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto kwa kuweka mazingira yao katika hali ya usafi, kwa kunawa mikono kwa maji na sabuni kwa kutmia vitakasa mikono.

“ Nawashukuru sana wadau kwa kutoa vifaa hivi na kwa baadhi ya maeneo mmeshiriki pia kutoa chakula, lakini pia niwashukuru sana viongozi wa dini mnafanya kazi kubwa sana, kwa mahubiri na mafundisho yenu juu ya hili janga la Covid -19,” alisema na kuwataka wadau wengine zaidi kujitokeza kwa ajili ya kutoa vifaa vingine zaidi.

Mhe.Mongella ameongeza kuwa  ugonjwa wa Corona ambao unaenea kwa kasi hivi sasa duniani ni hatari sana kwa maisha ya binadamu na kuwataka wananchi na watalaam kutofanya uzembe wa aina yoyote kwenye mapambano ya Corona.

“ Niwaombe viongozi wa dini, mashirika na taasisi zote tuendelee kuelimisha na kuwahamasisha wananchi namna ya kuendelea kuchukua tahadhari,” alisema na kuwashukuru Wakuu wa wilaya, Wakurugenzi watendaji, maafisa tarafa, madiwani na viongozi wa mitaa, vitongoji na vijiji kwa jinsi wanavyoendelea kujitoa katika kuwahamasisha wananchi namna bora ya kupambana na ugonjwa huo.

Akizungumza kwa niaba ya wadau waliokabidhi vifaa hivyo Mwakilishi kutoka Taasisi ya Hindu Nilesh Popat alisema wao wameamua kutoa vifaa hivyo ili kuunga juhudi za Serikali kwenye mapambano ya Corona.

“Mhe. Mkuu wa mkoa tumekuwa tukitembea mitaani bado tunaona mahitaji ni makubwa ya vifaa vinavyohitajika na ndiyo maana tumeamua kutoa vifaa hivi,” alisema Popat.

Kwa upande wake, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza (RMO) Dkt. Thomas Rutachuzibwa alizishukuru taasisi na wadau hao wa maendeleo kwa misaada ya vifaa hivyo ambayo itawawezesha wananchi kujikinga zaidi na maambukizi ya Corona.

Kwa upande wake Shehe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Hassan Kabeke aliwataka watanzania kuendelea kumuomba Mungu ili awanusuru na  janga hili la ugonjwa wa corona.

“ Tunawaombea pia hawa waliotoa misaada yao na tunataka watanzania waendelee kuchapa kazi huku wakijikinga na ugonjwa wa corona,” alisema.

Baadhi ya taasisi na mashirika yaliyotoa misaada hiyo ni taasisi ya Hindu Union Temple iliyotoa chupa 28 za 500 mls za sabuni za kunawia mikono, Nyanza Roads Network iliyotoa ndoo 100 za plastic za lita 20 zenye koki, Siri Guru Sigh Sabha ambao wametoa meza 10 za chuma, tenki 10 za lita 250 kila moja na viti 5-0 vya plastic.

Taasisi nyingine zilizokabidhi vifaa ni pamoja na Cocacola Company iliyotoa madumu 100 ya lita 20 kila moja na Henan Afro –Asia Geo Engineering Company iliyotoa barakoa 200, deto sabuni zenye ujazo wa  lita moja nne, vitakasa mikono chupa 48 kila chupa ikiwa na mls 250.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.