• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza kunafaika na Shs Bilioni 7.8 kutoka TASAF

Posted on: January 11th, 2023


Mkoa wa Mwanza unatarajia kunufaika na  Tshs. Bilioni 7.8 za miradi ya kunusuru Kaya masikini kwenye Wilaya zake 7 inayotekelezwa na Mfuko wa hifadhi ya Jamii (TASAF).

Akizungumza leo na uongozi wa TASAF kutoka Makao Makuu, Viongozi waandamizi kutoka Wizara ya Fedha, Benki ya Dunia na Ubalozi wa Norway, Katibu Tawala wa Mkoa w Mwanza Ndg. Balandya Elikana amesema Serikali ya Mkoa itasimamia imara utekelezaji wa Miradi hiyo ili malengo yaliyokusudiwa yatimie.

"Serikali ya awamu ya Sita imejipambanua kwa vitendo kumletea maendeleo mwananchi, hivyo Miradi kama hii yenye tija kwa Wananchi hasa zile Kaya masikini tuna kila sababu ya kuona unakuja na majibu chanya". Amesisitiza Mtendaji huyo wa Mkoa.

Balandya amesema katika fedha hizo tayari Tshs Bilioni 3.3 tayari zimekuja na kuanza utekelezaji wake kwa kujengwa Miundombinu ya Madarasa, Ofisi, Vituo vya afya pamoja na Barabara.

Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii, Shadrack Mziray amesema tangu mfuko huo uanze kazi rasmi nchini mwaka 2001 zaidi ya Tshs Bilioni 400 zimetolewa zilenga kuinua kiuchumi kaya masikini na kumekuwa na matokeo mazuri kupitia mradi huo.

"Wilaya ya Misungwi ambayo tutakuwa na kazi ya siku mbili ya kupitia miradi mbalimbali tayari kuna wanufaika 600 ambao wametoka hatua ya umasikini hivyo kazi iliyo mbele yetu ni kuhakikisha kundi kubwa la Watanzania wanafikia malengo ya Serikali". Amesema Mziray.

Kwa upande wake mwakilishi kutoka Benki ya Dunia Wout Soveur amebainisha kuwa, licha ya kutolewa fedha hizo lakini itakuwa ni kazi bure kama wanufaika na Miradi hiyo hawapatiwi elimu ya kutosha kuanzia  mpango wa Lishe bora na namna ya kujiongeza kipato cha familia.

Mpango wa kunusuru Kaya masikini ulizinduliwa Mkoani Mwanza Oktoba 2014 na kuanza kutekelezwa kwenye Wilaya zote Mkoani humo Julai 2015 ukiwa na jumla ya wanufaika 77,553.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.