• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA KUNG’ARA KUPITIA SANAA, RC MTANDA ATOA AHADI NZITO

Posted on: February 16th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda leo Februari 16, 2026 amekutana ofisini kwake na Msanii wa Filamu nchini, John Elisha maarufu kwa jina la Hamadi wa kombolela ambaye anatokea mkoani Mwanza.

Msanii huyo amefika kwa lengo la kujitambulisha rasmi, kutoa salamu pamoja na kuwasilisha baadhi ya tuzo alizozishinda katika mwaka 2025, ikiwa ni ishara ya mafanikio makubwa aliyoyapata kwenye tasnia ya filamu nchini.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Mtanda amempongeza John Elisha kwa juhudi, ubunifu na nidhamu katika kazi zake, akisema kuwa mafanikio yake ni fahari kwa Mkoa wa Mwanza na taifa kwa ujumla.

“Tunajivunia sana kuona vijana wetu wakifanya vizuri na kulitangaza jina la Mwanza kitaifa na kimataifa,” amesema Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Mtanda amemhakikishia msanii huyo pamoja na wasanii wote wanaotoka Mkoa wa Mwanza kuwa ofisi yake iko tayari kutoa ushirikiano na sapoti wakati wowote watakapohitaji msaada wa kiofisi au kimazingira katika kukuza vipaji vyao.

Aidha, amewataka wasanii kutosubiri hadi wakumbane na changamoto ndipo watafute msaada, bali wawe na utamaduni wa kufika ofisini kujadiliana, kushauriana na kujenga ushirikiano wa karibu na uongozi wa mkoa.

Sambamba na hayo, Mkuu wa Mkoa amepongeza tena John Elisha kwa kazi nzuri anayoifanya na kumtaka aendelee kuiwakilisha vyema Mwanza kupitia sanaa yake, huku akihamasisha wasanii wengine kuongeza juhudi, ubunifu na mshikamano.

Kwa upande wake, John Elisha ameshukuru kwa mapokezi na ushirikiano alioupata, akiahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha anaitangaza vyema Mwanza kupitia filamu na kazi zake nyingine za kisanii.

Mkutano huo unaonekana kuwa chachu mpya kwa wasanii wa Mkoa wa Mwanza, ukiashiria mwanzo wa ushirikiano imara kati ya uongozi wa mkoa na wadau wa sanaa katika kukuza vipaji na kuimarisha tasnia ya filamu nchini.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.