• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza wafaidika na vifaa vya uokoaji wakati wa majanga

Posted on: November 27th, 2018

Taasisi ya SUKOS KOVA Tanzania na Vodacom Tanzania wametoa vifaa vya uokoaji kama vile Vifaa vya kuzimia moto,Vifaa vya kuogelea vyenye thamani ya Shilingi  Milioni 120 wilayani Nyamagana,wanufaika wakiwa Jeshi la Zima moto, Wavuvi Shule ya Msingi Nyamagana, Sweya na Luchelele

Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Mkuuu wa wilaya ya Nyamagana Dkt Phillis Nyimbi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amewashukuru wadhamini wa vifaa hivyo kwa nia yao njema ya kusaidia watu wa kanda ya ziwa kuweza kujiokoa na majanga mbali mbali yanayoweza kujitokeza 

"Nimshukuru Mkurugenzi wa SUKOS KOVA na Vodacom Tanzania kwa nia yao njema ya kuwasaidia wana Mwanza.Hivi vifaa vikitumiwa ilivyokusudiwa itasaidia kupunguza na kutuepusha na baadhi ya majanga" amesema Dr Nyimbi

Aidha Dr Nyimbi amewataka watu wote waliopata vifaa hivyo vikatunzwe vyema na kutumika kwa maslai ya wengi na sio watu binafsi .

Akiongea kwa niaba ya Taasisi ya SUKOS KOVA foundation, Kamishna mstaafu wa Jeshi la Polisi Suleman Kova amesema ameguswa na kuona ni vyema Taasisi yake kujikita kutoa Elimu na vifaa kwa watanzania namna ya kujikinga na kujiokoa na majanga mbali mbali yanayotokea kwenye jamii zetu.

Hata hivyo Ndg Kova amewataka wadau wengine kuiga mfano wa Vodacom Tanzania na kuchangia vifaa mbali mbali kwa ajili ya kusaidia uokoaji wakati wa majanga,

Akitoa salam za Halmashauri ya Jiji la Mwanza Naibu Meya wa Jiji la Mwanza Mhe Bhiku kotecha amewashukuru wadau hao wa maendeleo kwa kulichagua Jiji la Mwanza na hususan Kata ya Nyamagana kuwa sehemu ya uzinduzi wa programu hiyo.

Pamoja na hilo, Mhe Kotecha amesema ataendelea kuwa balozi mzuri wa Vodacom Tanzania kutokana na Vodacom kutoa mchango mkubwa mara kwa mara kusaidia jamii.

Naibu meya ameendelea kuwaomba Vodacom Tanzania kuja kuwekeza kwenye uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu wilayani Nyamagana kwa kujenga majukwaa ya kukaa watu nao pia watapata fursa ya kutangaza matangazo yao ya biashara.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.