• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yaweka mikakati madhubuti katika kuimarisha Sekta ya Afya

Posted on: February 4th, 2020

Mkoa wa Mwanza umetangaza rasmi mkakati madhubuti  maeneo yote ya vivuko,bandari pamoja na uwanja wa ndege wa kimataifa  wa jijini Mwanza,kwa wageni wote wanaoingia mkoani humo  kutoka nje ya nchi kufanyiwa vipimo ili kubaini kama wameathirika na homa ya mafua makali yanayosababishwa na kirusi aina ya corona.

Afisa Afya Mkoa wa Mwanza Fungo Masalu akizungumza wakati wa  kujadili masuala ya lishe,afya ya uzazi hususani kwa mama mjamzito,mtoto pamoja na tahadhari ya magonjwa ya homa ya manjano na homa ya mafua makali yanayosababishwa na kirusi kipya aina ya corona yanayoendelea katika nchi mbalimbali alisema, mkakati uliopo ni kuimarisha mipaka ambayo inaingiza wageni.

“Tumeweka utaratibu wa kupima joto la mwili endapo mtu akiwa na joto homa kali atafanyiwa uchunguzi kubaini alipotokea yawezakuwa ametokea nchi iliyoathirika kwa sababu hali yake imeashiria kuwa na ugonjwa”alisema Masalu.

Aliongeza kuwa elimu ya afya itatolewa kwa umma hususani kipindi hiki kabla ya ugonjwa kufika nchini ili waweze kuzingatia kanuni za afya katika kujikinga na ugonjwa huo.

Awali ya yote Mratibu wa huduma ya mama na mtoto Mkoa wa Mwanza Cecilia Mrema,akitoa taarifa ya huduma ya afya ya uzazi na mtoto na hali ya vifo vya wazazi alisema, kwa mwaka jana mama wajawazito waliopoteza maisha kwa kutokwa na damu nyingi pamoja na kifafa cha mimba wakati wa kujifungua walifikia asilimia 40, hivyo wameweka mkakati ili kumaliza tatizo hilo ambapo hatua ya kwanza ni kuhakikisha upatikanaji wa damu unakuwa wa uhakika wakati wote.

Pia aliwataka wajawazito wote kupima wingi wa damu mapema ili ikibainika anakiwango kidogo cha damu waweze kumsaidia mapema akiwa kwenye huduma za wajawazito kabla ya wakati wake wa kujifungua endapo akichelewa hatutaweza kumsaidia katika hatua ya mwisho.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Dkt.Emmanuel Kipole kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella,alisema umasikini wa kipato,machafuko ya kisiasa  na sera zisizo tambua umuhimu wa lishe ndio chanzo kikubwa cha jamii kuwa na lishe duni.

Pia uelewa huo mdogo wa masuala ya lishe umechangia suala hilo kutokupewa kipaumbele katika mipango na bajeti hususani katika ngazi za halmashauri ambapo ndipo walipo watoto, vijana na wanawake wanaohitaji huduma bora za lishe .

“Serikali kwa kutambua lishe ni suala la kimaendeleo hapa Tanzania mapambano dhidi ya lishe duni yamekuwa ni moja wapo ya maeneo yaliyopewa kipaumbele katika mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano ulianza mwaka 2016-2017 na 2020-2021,”alisema Kipole.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.