• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA YAPANDA ZAIDI YA MITI ELFU 16 MAADHIMISHO SIKU ZA KUZALIWA RAIS SAMIA

Posted on: January 27th, 2026

Mkoa wa Mwanza wametumia siku ya tarehe 27 Januari, 2026 ambayo ni Siku ya Kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kupanda miti 16,000 katika maeneo mbalimbali ndani ya mkoa huo chini ya ushirikiano na Wakala wa Misitu nchini (TFS).

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Said Mtanda baada ya kushiriki zoezi la upandaji Miti zaidi ya 1200 katika Shule mpya ya Sekondari Kakebe- Igoma wilayani Nyamagana akiwa anahitimisha zoezi hilo aliloanza kwa kupanda Miti katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ilemela.

Mhe. Mtanda amesema Mkoa wa Mwanza umeungana na Mhe. Rais kufanya kazi za kijamii kwa kupanda miti ya matunda ili kwenda sambamba na afua ya lishe bora wa watoto kwa siku za baadaye pamoja na kusaidia katika uhifadhi wa mazingira.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kupanda miti kwenye mashamba na hata katika mazingira ya makaazi ili si tu kupanda miti bali kufanya sadaka kwa Mwenyezi Mungu kwa kujenga taifa la kijani kwa siku za usoni.

“Suala la kuhifadhi mazingira ni la kizalendo, mazingira bora yatajenga maisha bora na jamii ikihifadhi vizuri tutapata mvua za kutosha hivyo niwatake wananchi wote kupanda miti kwenye kaya zenu,” amesema Mkuu wa Mkoa.

Naye, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema pamoja kupanda miti katika Shule hiyo Wilaya imehamasisha upandaji miti katika maeneo yote hadi kwenye kaya na kwamba wanapanda miti ya matunda ili isiwe tu kwa ajili ya kivuli bali kuhamasisha lishe bora.

Aidha, ametumia wasaa huo kuishukuru Serikali kwa kuleta fedha nyingi za miradi huku akijinasibu kuwa upandaji miti kwenye shule hiyo mpya ya Kakebe utasaidia kuwaondolea wanafunzi adha ya kutembea zaidi ya Kilomita 5 kutoka Shamaliwa kwenda Igoma.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amechagiza hafla ya upandaji miti kwa kuendesha harambee kwa ajili ya kupata fedha Tshs. 1,800,000 za kuunganisha umeme na Maji kwenye shule hiyo ambapo zimepatikana Tshs. 1,350,800 papo hapo na amemuagiza Meneja wa TANESCO kupeleka umeme mara moja huku Maji yakifuata kwa kushirikiana na Mkurugenzi wa Jiji hilo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

    January 29, 2026
  • HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • TRA MWANZA YATOA MAFUNZO YA MFUMO JUMUISHI WA KODI ZA NDANI KWA WAFANYABIASHARA

    January 28, 2026
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI WA WIZARA YA ULINZI NA JKT MWANZA

    January 28, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.