• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWAUWASA washauriwa kuja na huduma sahihi na bora mradi wa maji Butimba

Posted on: November 9th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima ameishauri Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira kukaa chini na kufanya tathmini makini kuhusiana na idadi halisi ya wakazi wa Jiji hilo ili miradi yake ya maji iwanufaishe wananchi wote.

Akizungumza na uongozi wa Mamlaka hiyo mara baada ya kukagua maendeleo ya mradi wa chanzo cha maji Butimba,Mhe Malima amesema mara baada ya hesabu ya Sensa mwaka huu imeonesha Mwanza ina idadi ya watu milioni 4 hivyo mahitaji ya rasilimali hiyo itazidi kuwa kubwa.

"Nimemsikia hapa Meneja akisema mara baada ya mradi huo kukamilika utaweza kusambaza maji lita milioni 48 kwa siku hiyo haitoshi na Wananchi hawatawaelewa kuwa na mradi mkubwa namna hii halafu huduma ikawa bado hawaipati,ni lazima muone haja ya kufanya hesabu nzuri ili mradi huu uweze kutoa huduma kwa usahihi"amesema Mhe.Malima

Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha bado wakazi wa Jiji la Mwanza hasa waishio maeneo ya kwenye miinuko wanataabika kupata huduma ya maji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa mtambo na maji kupotea njiani kabla ya kumfikia mwananchi.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameutaka uongozi wa MWAUWASA kumletea taarifa ya kimaandishi kuhusiana

mradi huo kuchelewa kukabidhiwa tofauti na muda waliokubaliana ambao ni Disemba mwaka huu na sasa utakabidhiwa Juni mwakani.

"Alivyokuja Mhe.Makamu wa Rais Philip Mpango kuzindua mradi huu aliambiwa hadi Disemba utakuwa umekamilika,sasa leo mmnanipa taarifa tofauti yenye sababu zenu za msingi za vifaa kuchelewa kuletwa kutoka kwa msambazaji kutoka nje ya nchi".Amesema Mkuu huyo wa Mkoa

Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA,Mhandisi Leonard Msenyele amesema maagizo yote yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wameyapokea na kuyatekeleza ili malengo ya kuwapatia huduma bora wananchi yatimie.

Mradi wa chanzo cha maji Butimba upo chini ya mkandarasi SOGEA SATOM kutoka Ufaransa na umegharimu jumla ya Shilingi Bilioni 69.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.